عن أبي هريرة رضي الله عنه قال: كان رسول الله صلى الله عليه وسلم إذا كَبَّرَ في الصلاة سكت هُنَيْهَةً قبل أن يقرأ، فقلت: يا رسول الله، بأبي أنت وأمي، أَرَأَيْتَ سُكُوتَكَ بين التكبير والقراءة: ما تقول؟ قال: أقول: اللَّهُمَّ باعد بيني وبين خطاياي كما باعدت بين المشرق والمغرب. اللهم نَقِّنِي من خطاياي كما يُنَقَّى الثوب الأبيض من الدَّنَسِ. اللهم اغْسِلْني من خطاياي بالماء والثَّلْجِ وَالْبَرَدِ.
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Alikuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- anapotoa takbira katika swala ananyamaza kidogo kabla hajaanza kusoma, nikasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, nimuweka fidia baba yangu na mama yangu, Hebu nieleze kunyamaza kwako kati ya takbira na kisomo: Ni nini unasema: Akasema: Ninasema: Allaahumma baaid bainiy -Ewe Mwenyezi Mungu weka mbali baina yangu- wa baina khatwaayaaya -na baina ya makosa yangu- kamaa baa a'tta bainal mashriqi wal maghribi -kama ulivyoweka mbali baina ya mashariki na magharibi. Allaahumma naqqiniy- Ewe Mwenyezi Mungu nitakasa mimi- min khatwaayaaya -kutokana na makosa yangu- kamaa yunaqqath-thaubul abyadhwa -kama inavyotakaswa nguo nyeupe- minad danasi -kutokana na uchafu. Allaahumma ghsilniy -Ewe Mwenyezi Mungu nioshe mimi- min khatwaayaaya -kutokana na makosa yangu- bil maai wath thalji wal baradi -kwa maji na barafu na baridi.
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Alikuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- anapotoa takbira kwaajili ya swala, takbira ile ya kufungua swala, anashusha sauti yake muda kidogo kabla ya kusoma suratul-fatiha. Na walikuwa maswahaba wanajua kuwa kuna kitu anachokisoma katika kunyamaza huku, ima kwasababu swala yote ni dhikri (kumtaja Mwenyezi Mungu) hakuna kunyamaza bila kusikiliza, na ima kwasababu ya harakati za Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- wakajua anasoma, na kwasababu ya pupa ya Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- juu ya elimu na sunna akasema: Nakutolea fidia ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu baba yangu na mama yangu, nini unasema katika kimya hiki ambacho kiko kati ya takbira na kisomo? akasema: Ninasema: Ewe Mwenyezi Mungu weka mbali kati yangu na makosa yangu kama ulivyoweka mbali kati ya mashariki na magharibi, ewe Mwenyezi Mungu nisafishe kutokana na makosa yangu, kama inavyosafishwa nguo nyeupe kutokana na uchafu, ewe Mwenyezi Mungu nioshe kutokana na makosa yangu kwa maji na theluji na baridi". Na dua hii iko katika kiwango cha juu sana cha kufaa katika sehemu hii tukufu, mahala pa kunong'ona, kwasababu mwenye kuswali anaelekea kwa Mwenyezi Mungu -Mtukufu- katika kumfutia madhambi yake na aweke mbali baina yake na baina ya hayo madhambi, umbali ambao haiwezekani kukutana, kama ambavyo hazikutani mashariki na magharibi milele, na ayaondoe kwake madhambi na makosa na amsafishe nayo, kama unavyoondolewa uchafu katika nguo nyeupe, na amuoshe kutokana na makosa yake, na aupoze muwako wake na joto lake, kwa hivi vitakasa vya baridi; Maji, Na theluji, na baridi. Na kufananisha huku kuko katika kiwango cha juu zaidi cha kuendana na hilo. Na kwa dua hii mtu anakuwa kaepukana na athari ya madhambi, atasimama mbele ya Mwenyezi Mungu Mtukufu akiwa katika hali ya ukamilifu zaidi, na lililo bora zaidi ni mtu azifanyie kazi dua zote sahihi za ufunguzi zilizothibiti, wakati mwingine anaifanyia kazi hii, na wakati mwingine hii, hata kama hadithi hii ya Abuu Huraira ndiyo sahihi zaidi. Na Mwenyezi Mungu ndiye mjuzi zaidi.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama
Ziada