عن ثَوْبَان رضي الله عنه قال: كان رسول الله صلى الله عليه وسلم إذا انْصَرف من صلاته اسْتَغْفَر ثلاثا، وقال: «اللهُمَّ أنت السَّلام ومِنك السَّلام، تَبَارَكْتَ يا ذا الجَلال والإكْرَام».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Thauban -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Alikuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu -Rehma na Amani ziwe juu yake- anapomaliza swala yake anataka msamaha mara tatu, na anasema: Allaahumma antas salaam, waminkas salaam, Tabaarakta yaa dhal-jalaali wal-ikraam (Ewe Mwenyezi Mungu hakika wewe ni Amani, na Amani hutoka kwako, umetakasika Ewe mwenye Utukufu na ukarimu).
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

katika hadithi kuna ubainifu wa kupendeza kusema mwenye kuswali baada ya kumaliza swala: Namuomba Mwenyezi Mungu msamaha, Namuomba Mwenyezi Mungu msamaha, Namuomba Mwenyezi Mungu msamaha. Kisha asema dua hii: "Allaahumma antas salaam, waminkas salaam, Tabaarakta yaa dhal-jalaali wal-ikraam". Na kuna dua zingine zilizokuja katika hadithi zingine katika yale yanayosemwa baada ya swala.

Kufanya Tarjama: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibaghali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai Kijapani
Kuonyesha Tarjama

Faida nyingi

  1. Hapa kuna jibu kwa mwenye kusema kuwa: mwenye kuswali anatakiwa kutoa takbira (yaani kusema: Allaahu Akbar) baada ya swala.
  2. Kuna uthibitisho wa jina la "Assalaam" (Amani) kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu- na sifa yake, yeye amesalimika na kila mapungufu na aibu, na yeye ndiye mgawaji wa Amani kwa waja wake kutokana na shari za dunia na Akhera.
Ziyada