عن عائشة رضي الله عنها ، قالت: افْتَقَدْتُ النبي صلى الله عليه وسلم ذات ليلة، فَتَحَسَّسْتُ، فإذا هو راكع -أو ساجد- يقول: «سُبْحَانَك وبِحَمْدِكَ، لا إله إلا أنت» وفي رواية: فَوَقَعَتْ يَدِي على بَطن قدميه، وهو في المسجد وهما مَنْصُوبَتَانِ، وهو يقول: «اللَّهُمَّ إني أَعُوذ بِرِضَاك من سَخَطِك، وبِمُعَافَاتِكَ من عُقُوبَتِكَ، وأعُوذ بِك مِنْك، لا أُحْصِي ثَناءً عليك أنت كما أَثْنَيْتَ على نفسك».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Aisha - Radhi za Allah ziwe juu yake-Amesema:alimkosa Mtume- Rehema na Amani ziwe juu yake- katika usiku mmoja,hakumpata kitandani kwake;akaenda akimtafuta na alikuwa akidhani -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kuwa amekwenda kwa baadhi ya wake zake,kisha akampata -Rehema na Amani ziwe juu yake- naye akiwa amerukuu au amesujudu,akisema: Umetakasika wewe na sifa njema ni zako,hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa wewe,Na katika riwaya nyingine: ukaangukia mkono wake kwenye nyayo zake na akiwa msikitini na amezisimamisha nyayo mbili hizo alimsikia akisema: "Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi najilinda kwa radhi zako kutokana na hasira zako" Yaani: ninaomba kinga kwa radhi zako kuepushwa na hasira zako,."na ninajilinda kwa msamaha wako kutokana na adhabu zako,"Na ninajilinda kwako kwa kinga yako,nasiwezi kuzidhibiti shukurani zako zote
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Katika hadithi hii anaeleza Aisha -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kuwa yeye alimkosa Mtume- Rehema na Amani ziwe juu yake- katika usiku mmoja,hakumpata kitandani kwake;akaenda akimtafuta na alikuwa akidhani -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kuwa amekwenda kwa baadhi ya wake zake,kisha akampata -Rehema na Amani ziwe juu yake- naye akiwa amerukuu au amesujudu,akisema: Umetakasika wewe na sifa njema ni zako,hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa wewe, yaani: ninakutakasa na yote yasiyofaa kwako,na ninakushukuru kwa matendo yako yote,na wewe ndiye mwenye sifa na shukurani za milele,Hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki ispokuwa wewe. Na katika riwaya nyingine: Nikuwa yeye alipokuwa akimtafuta ukaangukia mkono wake kwenye nyayo zake; kwasababu hapakuwa na mwanga wa kuweza kumuona -Rehema na Amani ziwe juu yake-,bali alikuwa akimtafuta kwa kupapasa kwa mikono yake mpaka ukaangukia mkono wake kwake, naye akiwa kasujudu,pindi alipompata -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- alimsikia akisema: "Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi najilinda kwa radhi zako kutokana na hasira zako" Yaani: ninaomba kinga kwa radhi zako kuepushwa na hasira zako,na siku zote jambo hutibiwa kwa kinyume chake, hasira kinyume chake ni radhi, anaomba kinga katika radhi za Mwenyezi Mungu Mtukufu kutokana na hasira zake."Na kwa usalama wako kutokana na adhabu zako" Na ninajilinda kwa msamaha wako kutokana na adhabu zako."Na ninajilinda kwako kwa kinga yako" Yaani ninaomba kinga kwa Mwenyezi Mungu kutokana na Mwenyezi Mungu Mtukufu na hii; ni kwasababu hakuna kuokoka wala pakumkimbia Mwenyezi Mungu isipokuwa kwake, hakuna yeyote awezaye kukuokoa na adhabu za Mwenyezi Mungu isipokuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu."Siwezi kuzidhibiti shukurani zako zote " Yaani siwezi kukusifia kwa yale unayostahiki kwa vyovyote nitakavyopitiliza katika kukusifu,bali mimi nina mapungufu kiasi cha kuweza kufikia sifa zangu kwako kiwango unachostahiki."Wewe kama ulivyojisifia juu ya nafsi yako" Yaani ninakusifia sifa kama ulivyojisifu hakuna awezaye kudhibiti sifa juu yake kama alivyojisifia Mwenyezi Mungu juu ya nafsi yake.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kireno
Kuonyesha Tarjama
Ziada