عن جابر رضي الله عنه قال: سمعت رسول الله صلى الله عليه وسلم يقول: «أفضل الذِّكر: لا إله إلا الله».
[حسن] - [رواه الترمذي والنسائي في الكبرى وابن ماجه]
المزيــد ...
Kutoka kwa Jaabir Radhi za Allah ziwe juu yake amesema: nilimsikia Mtume Muhammad Rehma na Amani za Allah ziwe juu yake akisema: "Dhikri bora ni: Laa ilaaha ila LLah".
Ni nzuri - Imepokelewa na Ibnu Maajah
Anatueleza Mtume rehema na Amani zimfikie yakuwa dhikri bora ni "Laa ilaaha illa llaah" Hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu, na katika hadithi nyingine: maneno bora niliyoyasema mimi na Manabii kabla yangu "Laa ilaaha illa llaah wahdahu Laa shariika lahu" (Hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu yeye pekee asiye na mshirika). Na hakuna shaka kuwa neno hili ni neno kubwa, imesimama kupitia hilo ardhi na mbingu, na vimeumbwa kwaajili yake viumbe vyote, na kwao Mwenyezi Mungu Mtukufu akatuma Mitume, na akateremsha vitabu vyake, na akaleta sheria zake, na kwaajili yake ikasimikwa njia nyembamba (swiraatwa), na yakawekwa mafaili, na likasimama soko la pepo na moto, na maana yake Hakuna aabudiwaye kwa haki ispokuwa Mwenyezi Mungu, na sharti zake ni saba: Elimu na yakini na kukubali na kutii na kusadikisha na utakasifu wa moyo (Ikhlaswi) na mapenzi, na kutokana na hilo wataulizwa wa mwanzo na wa mwisho, hautonyanyuka unyayo wa mja mbele ya Mwenyezi Mungu mpaka aulizwe maswali mawili: Mlikuwa mkiabudu nini? na mliwajibu nini Mitume?. Hivyo jawabu la kwanza ni kwa kuihakikisha "Laa ilaaha illa llaah" kwa kujua na kuikubali na kuifanyia kazi. Na jawabu la pili ni kwa kuhakikisha "Kuwa Muhammadi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu kwa kujua na kukiri na kutii na kukubali. Amesema Mtume rehema na Amani zimfikie: "Umejengeka Uislamu juu ya mambo matano: Kushuhudia kuwa Hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu na kuwa Muhammadi ni Mjumbe wa Mwenyezi Mungu.