عن سَمُرة بن جُنْدَب رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : «أحب الكلام إلى الله أربع لا يَضُرُّك بِأَيِّهِنَّ بدأت: سُبْحَانَ الله، والحمد لله، ولا إله إلا الله، والله أكبر».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...
Kutoka kwa Samra bin Jundab Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake Amesema: Amesema Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake-: "Maneno yanayopendeka zaidi kwa Mwenyezi Mungu ni manne, haikudhuru kwa lolote utakaloanza nalo: Sub-haanallah (Ametakasika Mwenyezi Mungu) Al-hamdulillaah (Kila sifa njema zinamstahiki Mwenyezi Mungu), Na, Laa ilaaha illa llaah, (Hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu), Na Allahu Akbar (Mwenyezi Mungu Mkubwa)".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim
Hadithi inaelezea ubora wa ibara hizi nne, nakuwa ni katika maneno yanayopendeka zaidi kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, kwa kukusanya kwake mambo makubwa, nako ni kumtakasa Mwenyezi Mungu Mtukufu, Na ni kumsifu kwa yote yanayolazimu kwake katika sifa za ukamilifu, na kumpwekesha kwa upweke wake na ukubwa, nakuwa ubora wake na kupata thawabu zake hakuna ulazima wa kuyapangilia kama yalivyokuja katika hadithi.