عن أبي هريرة رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : «أكْثَرُ مَا يُدْخِلُ الْجَنَّةَ تَقْوَى اللَّهِ وَحُسْنُ الْخُلُقِ».
[حسن صحيح] - [رواه الترمذي]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake Amesema: Amesema Mtume Rehema na Amani zimfikie:"Vinavyowaingiza watu kwa wingi peponi ni uchamungu na tabia njema. ".
Ni nzuri na nisahihi - Imepokelewa na Imamu Tirmidhiy

Ufafanuzi

Katika hadithi kuna dalili ya ubora wa uchamungu, nakuwa ni sababu ya kuingia peponi, na vile vile katika ubora wa tabia njema, nakuwa mambo haya mawili (Uchamungu na tabia njema) ni katika sababu kubwa zinazomuingiza mja peponi.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Nikuwa kuingia peponi kunakuwa kupitia sababu na matendo sheria imeyataja.
  2. Katika sababu za kuingia peponi ni sababu zinazoambatana na Mwenyezi Mungu miongoni mwazo ni hizi katika hadithi: "Kumcha Mwenyezi Mungu" Na kuna sababu zinazoambatana na viumbe, na miongoni mwazo ni hizi katika hadithi: "Tabia njema".
  3. Katika hadithi kuna dalili ya ubora wa uchamungu, nakuwa ni sababu ya kuingia peponi.
  4. Ubora wa tabia njema juu ya ibada nyingi, nakuwa pia ni katika sababu za kuingia peponi.