عن سهل بن سعد رضي الله عنه عن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال:
«مَنْ يَضْمَنْ لِي مَا بَيْنَ لَحْيَيْهِ وَمَا بَيْنَ رِجْلَيْهِ أَضْمَنْ لَهُ الْجَنَّةَ».

[صحيح] - [رواه البخاري] - [صحيح البخاري: 6474]
المزيــد ...

Imepokelewa Kutoka kwa Sahal Ibn Sa'd -Radhi za Allah ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-:
"Yeyote atakayenidhaminia mimi vilivyo kati ya Taya mbili na vilivyo kati ya miguu yake ninampa dhamana ya Pepo".

[Sahihi] - [Imepokelewa na Al-Bukhaariy] - [Swahiih Al Bukhaariy - 6474]

Ufafanuzi

Anaeleza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuhusu mambo mawili nayo muislamu basi ataingia Peponi,
La kwanza: Kuhifadhi ulimi kutozungumza yale yenye kumchukiza Allah Mtukufu,
La pili: Kuhifadhi tupu kutotumbukia katika machafu;
Kwa sababu viungo viwili hivi hukithiri kutokea maasi kwavyo.

Katika Faida za Hadithi

  1. Kuhifadhi ulimi na tupu ni njia ya kuingia Peponi.
  2. Umetajwa mahususi ulimi na utupu; kwa sababu ndio vyanzo vikuu vya balaa kwa mwanadamu katika dunia na Akhera.
Kuonyesha Tarjama
Lugha: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Ziada (67)