Aina ndogo

Orodha ya Hadithi

Atakaye shuhudia kuwa hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu yeye pekee asiye na mshirika nakuwa Muhammadi ni mjumbe wake na ni mja wake, nakuwa Issa ni mja wa Mwenyezi Mungu na Mtume wake na neno lake alilolipeleka kwa Mariam na ni roho toka kwake, na pepo ni kweli na moto ni kweli, Atamuingiza Mwenyezi Mungu peponi kulingana na yale aliyokuwa nayo katika matendo.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayekutana na Mwenyezi Mungu hali yakuwa hamshirikishi na chochote ataingia peponi, na atakaye kutananaye hali yakuwa anamshirikisha na chochote ataingia motoni.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Yeyote atakaye nidhamini kuhifadhi ulimi wake na tupu yake nitamdhamini kuingia peponi.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Pepo iko karibu na mmoja wenu kuliko hata kisigino cha kiatu chake, na moto mfano huo huo.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Umezingirwa moto kwa mambo yenye kutamanisha, na imezingirwa pepo kwa yenye kuchukiza.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Vinavyowaingiza watu kwa wingi peponi ni uchamungu na tabia njema.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mwenyezi Mungu alipoumba Pepo na Moto alimtuma Malaika Jibril -Amani iwe juu yake- aende peponi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ee fulani, una nini wewe? kwani hukuwa unaamrisha mema na unakataza mabaya? atasema: Ndivyo, nilikuwa nikiamrisha mema na wala siyafanyi, na ninakataza mabaya na ninayafanya
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hili ni jiwe lililotupwa motoni tangu miaka sabini, anaporomoka motoni sasa hivi mpaka kaishia katika kina chake ndio maana mkasikia kishindo chake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Nilikuwa kwa Saidi bin Jubair akasema: Ni nani kati yenu aliyeiona nyota iliyodondoka jana usiku? Nikasema: Mimi, kisha nikasema: Ama mimi sikuwa katika swala, lakini niling'atwa (na Nge)
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika peponi kuna daraja mia moja kaziandaa Mwenyezi Mungu kwaajili ya wenye kupigana katika njia ya Mwenyezi Mungu kati ya daraja mbili ni kama masafa ya baina ya mbingu na ardhi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayetoa vitu vya namna mbili katika njia ya Mwenyezi Mungu huitwa katika milango ya pepo, ewe mja wa Mwenyezi Mungu hii ni kheri, atakayekuwa miongoni mwa watu wa swala ataitwa katika mlango wa swala, atakayekuwa katika watu wa jihadi ataitwa katika mlango wa jihadi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Hakika mwenye adhabu nyepesi zaidi katika watu wa motoni siku ya kiyama, ni mtu atawekewa ndani ya nyayo zake makaa mawili ya moto, utakuwa ukitokota kupitia hayo ubongo wake, na yeye atakuwa akiona kuwa hakuna mtu mwenye adhabu kali zaidi yake, na hakika kumbe yeye ndiye mwenye adhabu nyepesi kuliko wao
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Aina mbili za watu ni miongoni mwa watu wa motoni, sijawaona (katika zama zake Mtume), watu walio na mijeledi mithili ya mikia ya Ng'ombe wakiwapiga watu, na wanawake waliovaa na wako uchi, wanenguaji wakatikaji
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mauti yataletwa yakiwa kama dume la Kondoo mwenye rangi mchanganyiko ya weusi na weupe
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Moto wenu wa Dunia ni sawa na sehemu tu ya sabini itokanayo na moto wa Jahannam
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa