عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ رَضيَ اللهُ عنهُ أَنَّ رَسُولَ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ:
«إِنَّ فِي الْجَنَّةِ لَسُوقًا، يَأْتُونَهَا كُلَّ جُمُعَةٍ، فَتَهُبُّ رِيحُ الشَّمَالِ فَتَحْثُو فِي وُجُوهِهِمْ وَثِيَابِهِمْ، فَيَزْدَادُونَ حُسْنًا وَجَمَالًا، فَيَرْجِعُونَ إِلَى أَهْلِيهِمْ وَقَدِ ازْدَادُوا حُسْنًا وَجَمَالًا، فَيَقُولُ لَهُمْ أَهْلُوهُمْ: وَاللهِ لَقَدِ ازْدَدْتُمْ بَعْدَنَا حُسْنًا وَجَمَالًا، فَيَقُولُونَ: وَأَنْتُمْ وَاللهِ لَقَدِ ازْدَدْتُمْ بَعْدَنَا حُسْنًا وَجَمَالًا».
[صحيح] - [رواه مسلم] - [صحيح مسلم: 2833]
المزيــد ...
Imepokelewa kutoka kwa Anas bin Maliki radhi za Allah ziwe juu yake: Ya kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani ziwe juu yake amesema:
"Hakika Peponi kuna Soko, watakuwa wakienda hapo kila siku ya Ijumaa, basi utavuma upepo wa kaskazi utawamwagikia katika nyuso zao na nguo zao, na hapo wataongezeka uzuri na urembo, watarudi kwa familia zao wakiwa wameongezeka uzuri na urembo, watasema kuwaambia: Wallahi mmezidi uzuri na urembo baada yetu, watasema: Na nyinyi Wallahi hakika mmezidi uzuri na urembo baada yetu".
[Sahihi] - [Imepokelewa na Imamu Muslim] - [صحيح مسلم - 2833]
Ameeleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake ya kwamba Peponi kuna sehemu watu watakuwa wakikusanyika hapo, hapatokuwa na kuuza wala kununua, bali watakuwa wakichukua kutoka hapo wanachokitaka, watakuwa wakienda hapo kwa kiasi cha siku saba, utavuma upepo wa kaskazi, utatikisa katika nyuso zao na nguo zao, wataongezeka uzuri na urembo, watarudi kwa familia zao wakiwa wameongezeka uzuri na urembo, watasema kuwambia: Wallahi hakika mmezidi uzuri na urembo baada yetu, na wao watasema: Na nyinyi Wallah hakika mmezidi uzuri na urembo baada yetu.