عَنْ أَبِي سَعِيدٍ الْخُدْرِيِّ رَضيَ اللهُ عنهُ عَنِ النَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ:
«إِنَّ فِي الْجَنَّةِ شَجَرَةً يَسِيرُ الرَّاكِبُ الْجَوَادَ الْمُضَمَّرَ السَّرِيعَ مِائَةَ عَامٍ مَا يَقْطَعُهَا».
[صحيح] - [متفق عليه] - [صحيح مسلم: 2828]
المزيــد ...
Imepokelewa kutoka kwa Abii Saidi Al-Khudry radhi za Allah ziwe juu yake kutoka kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake amesema:
"Hakika ndani ya Pepo kuna mti ambao anatembea aliyepanda kipando madhubuti chenye uimara na kasi kubwa ya kukimbia kwa muda wa miaka mia moja na haumalizi (kuuvuka) mti huo".
[Sahihi] - [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim] - [صحيح مسلم - 2828]
Ameeleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake ya kwamba peponi kuna mti ambao anatembea chini yake aliyepanda Farasi aliyeandaliwa kwa mashindano, na mwenda kasi zaidi katika kukimbia kwake miaka mia moja lakini hafiki mwisho wa yanakolalia matawi yake.