عن أبي هريرة رضي الله عنه أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: «حُجِبت النار بالشهوات، وحُجبت الجنة بالمَكَاره»متفق عليه وهذا لفظ البخاري.
وفي رواية لهما: «حُفَّت» بدل «حُجِبت».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Huraira Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake yakwamba Mtume rehema na Amani zimfikie Amesema: "Umezingirwa moto kwa mambo yenye kutamanisha, na imezingirwa pepo kwa yenye kuchukiza" Hadithi Muttafaqun alaihi na tamko ni la Bukhari. Na katika riwaya yao nyingine: "Imezungukwa".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim
Maana ya hadithi: Nikuwa njia inayofikisha peponi imezungukwa na mambo anayoyachukia mwanadamu; kwasababu asili ya nafsi siku zote inaegemea katika raha. Na hivyo hivyo moto hawezi kuuingia mpaka ayavunje yale yaliyo kati yake na moto kwa kuyaendea maharamisho na kujiweka mbali na utiifu, atakayevunja kizuizi atakifikia kilichokingwa, akavunja kizuizi cha pepo kwa kuyaendea machukizo na akavunja kizuizi cha moto kwa kuyaendea matamanio, na ama machukizo inaingia humo juhudi katika ibada na kudumu juu yake na kuvumilia tabu zake na kuzuia hasira na kusamehe na upole na sadaka na wema kwa yule aliyekukosea na kusubiri katika matamanio na mfano wa hayo. Nafsi inaweza kuchukia kudumu katika swala; kwasababu ya yale yaliyomo kama kutoa juhudi na kuachana na yale ambayo nafsi inayatamani katika mambo ya kidunia, na inaweza kuchukia jihadi na inaweza kuchukia kutoa sadaka ya mali, kwasababu nafsi imeumbiwa kupenda mali, na mengineyo katika mambo ya kheri, atakapoyavunja mtu matamanio yake na akaenda kinyume na yale ambayo nafsi yake inayatamani, kwa kutekeleza maamrisho na kuyaepuka makatazo, inakuwa hiyo ni sababu ya kuingia peponi na kuwa mbali na moto. Na ama matamanio ambayo moto umezungukwa nayo, kimuonekano ni yale matamanio ya maharamisho kama pombe na zinaa na kumtazama mwanamke asiyehalali yako, na kusengenya na kutumia vitu vyenye kupumbaza na mfano wake, na ama matamanio ya halali hayaingii katika hili, lakini haipendezi kuyakithirisha, kwa kuogopea yasijekusogea katika maharamisho, au yakautia ugumu moyo au yakamshughulisha na mambo ya kheri, au yakapelekea kipaumbele cha kuipata Dunia.