عن أبي سعيد وأبي هريرة رضي الله عنهما مرفوعاً: «ما يُصيب المسلم من نَصب، ولا وصَب، ولا هَمِّ، ولا حَزن، ولا أَذى، ولا غَمِّ، حتى الشوكة يُشاكها إلا كفر الله بها من خطاياه».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Saidi na Abuu Huraira Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- Hadithi Marfu'u: "Haumpati muislamu uchovu wala maradhi, wala msongo, wala huzuni, wala udhia, wala shida, hata mwiba unaomchoma, ispokuwa anamfutia Mwenyezi Mungu kupitia hilo makosa yake".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Maana ya hadithi hii: nikuwa yale yanayomfika muislamu miongoni mwa maradhi na misongo ya mawazo na huzuni na matatizo na misiba na shida na hofu na kufazaika ispokuwa yanakuwa hayo ni kafara ya madhambi yake na ni kifutio cha makosa yake. Na akizidisha mtu juu ya hapo: na kuvumilia na kutaraji, yaani kutaraji malipo, atakuwa na malipo pia pamoja na hili. Matatizo huwa yana namna mbili: Wakati mwingine: Anapopatwa mwanadamu anakumbuka malipo na anataraji malipo kwa Mwenyezi Mungu katika mtihani huo, kunakuwa ndani yake na faida mbili: Kufutiwa madhambi na ziada ya mema. Na wakati mwingine hulisahau hili, kikadhikika kifua chake, na akapatwa na unyonge au chochote mfano wa hicho, na anaisahau nia ya kutaraji malipo na thawabu kwa Mwenyezi Mungu inakuwa kwa hilo ni kufutiwa madhambi yake, hivyo basi yeye anafaidika kwa kila namna. Na ima anaweza kufaidika kwa kufutiwa makosa, na ni kufutiwa makosa bila ya kupata malipo; kwasababu hakunuia chochote na wala hakuvumilia na wala hakutaraji malipo, Na ima afaidike kwa mambo mawili: Kufutiwa makosa na kupata thawabu kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu kama ilivyotangulia. Na kwaajili hiyo inatakiwa mtu anapopatwa hata na mwiba, akumbuke kutaraji malipo kutoka kwa Mwenyezi Mungu juu ya tatizo hilo, ili alipwe juu ya hilo, pamoja na kufutiwa kwake madhambi. Na hii ni katika neema za Mwenyezi Mungu Mtukufu na ukarimu wake, Kiasi ambacho anamjaribu muumini kisha anamlipa juu ya mtihani huu au anamfutia makosa yake. Tahadhari: Kufutwa kwa makosa kunakuwa kwa madhambi madogo, si makubwa ambayo hakuna kinachoweza kuyaondoa ispokuwa ni toba ya kweli.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Ndani ya hadithi nikuwa maradhi na mitihani mingineyo, inayompata muumini: inamsafisha kutokana na madhambi na makosa hata kama itakuwa midogo.
  2. Kuna bishara kubwa kwa waislamu; kwasababu hakuna muislamu yeyote ispokuwa anapatwa na mitihani hii.
  3. kuna kunyanyuliwa daraja kupitia mambo haya na kuongezewa mema.
  4. Kufutiwa madhambi kunaishia katika baadhi ya makosa, nayo ni yale madogo, ama madhambi makubwa ni lazima kuleta toba.