عن طلحة بن عبيد الله رضي الله عنه قال: جاء رجل إلى رسول الله صلى الله عليه وسلم من أهل نَجْدٍ ثَائِرُ الرأس نَسْمَع دَوِيَّ صوته، ولا نفقه ما يقول، حتى دَنَا من رسول الله صلى الله عليه وسلم فإذا هو يَسأل عن الإسلام، فقال رسول الله صلى الله عليه وسلم : «خمس صَلَواتٍ في اليوم واللَّيلة» قال: هل عليَّ غَيْرُهُنَّ؟ قال: «لا، إلا أن تَطَّوَّعَ» فقال رسول الله صلى الله عليه وسلم : «وصيام شهر رمضان» قال: هل عليَّ غَيْرُه؟ قال: «لا، إلا أن تَطَّوَّعَ» قال: وذكر له رسول الله صلى الله عليه وسلم الزكاة، فقال: هل عليَّ غَيْرُهَا؟ قال: «لا، إلا أن تَطَّوَّعَ» فأَدْبَر الرَجُل وهو يقول: والله لا أَزيد على هذا ولا أنْقُص منه، فقال رسول الله صلى الله عليه وسلم : «أَفْلَح إن صَدَق».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Twalha bin Ubaidillahi -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Alikuja mtu mmoja kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kutoka maeneo ya Najid, kichwa chake kikiwa kimetimka, tunasikia mvumo wa sauti yake, na wala hatuelewi anasema nini, mpaka akasogea karibu kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- ghafla akaanza kuuliza kuhusu uislamu, akasema Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- "Swala tano mchana na usiku" Akasema: Je kuna la wajibu juu yangu zaidi ya hayo? Akasema: "Hapana ila kama utajitolea" Akasema Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- "Na kufunga mwezi wa ramadhani" Akasema: Je kuna la wajibu juu yangu zaidi ya hilo? Akasema: "Hapana ila kama utajitolea" Akasema na akamtajia Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- zaka, akasema: Je kuna la wajibu juu yangu zaidi ya hilo? Akasema: "Hapana ila kama utajitolea" Akageuka kuondoka yule bwana huku akisema: Wallahi sitozidisha juu ya hili wala sitopunguza, Akasema Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- "Kafaulu kama akiwa mkweli".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Alikuja mtu mmoja kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- katika watu wa Najid, nywele zake zikiwa zimetimka na sauti yake iko juu, na hawakuelewa maswahaba -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- maneno yake mpaka aliposogea karibu ya Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake-, akamuuliza kuhusu majukumu ya kisheria ndani ya uislamu, akaanza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- na swala, akamueleza kuwa Mwenyezi Mungu kamfaradhishia swala tano katika kila mchana na usiku, akasema: Je kuna kingine kinachonilazimu katika swala nje ya swala tano?. Akasema: Hakikulazimu chochote zaidi ya swala tano, na miongoni mwa hizo ni swala ya ijumaa; kwasababu ni katika swala za usiku na mchana, isipokuwa kama utajitolea kama ziada juu ya yale aliyokuwajibishia Mwenyezi Mungu juu yako, hilo ni bora. Kisha akasema Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- na miongoni mwa yale aliyokuwajibishia Mwenyezi Mungu juu yako- ni kufunga mwezi wa ramadhani, akasema yule bwana: je kuna lolote la wajibu katika kufunga zaidi ya ramadhani? Akasema hakikulazimu chochote katika kufunga zaidi ya ramadhani, isipokuwa kama ukijitolea kufunga, kama kufunga juma tatu na Alhamisi na siku sita za shawwal na Arafa, basi hilo ni bora. Kisha akamtajia Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- zaka, akasema yule bwana: Je ninalazimika kutoa chochote katika sadaka baada ya kutoa zaka ya mali? Akasema: Hakikulazimu chochote isipokuwa ukijitolea mwenyewe bila kulazimishwa, basi hilo ni bora. Na baada ya kusikia yule bwana toka kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- majukumu ya kisheria, akageuka akaondoka na akaapa kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu kuwa atashikamana na yale aliyomuwajibishia Mwenyezi Mungu bila kuongeza wala kupunguza. Basi akasema Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- baada ya hayo: akiwa mkweli huyu bwana katika haya aliyoyaapia, basi atakuwa ni mwenye kufaulu na kachukua sababu ya kufaulu, nayo ni kuyatekeleza yale aliyoyawajibisha Mwenyezi Mungu Mtukufu juu yake.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kichina Kifursi Kihindi Kisin-hala Kikurdi Kireno الدرية
Kuonyesha Tarjama