عن ابن عباس رضي الله عنهما : أن رسول الله صلى الله عليه وسلم لما بعث معاذا إلى اليمن قال له: "إنك تأتي قوما من أهل الكتاب، فليكن أولَ ما تدعوهم إليه شهادة أن لا إله إلا الله" -وفي رواية: "إلى أن يوحدوا الله-، فإن هم أطاعوك لذلك فأعلمهم أن الله افترض عليهم خمس صلوات في كل يوم وليلة، فإن هم أطاعوك لذلك فأعلمهم أن الله افترض عليهم صدقة تؤخذ من أغنيائهم فَتُرَدُّ على فقرائهم، فإن هم أطاعوك لذلك فإياك وكَرَائِمَ أموالِهم، واتق دعوة المظلوم فإنه ليس بينها وبين الله حجاب".
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Ibn Abbas radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao, yakwamba Mtume rehema na Amani zimfikie alipomtuma Mua'dhi kwenda Yemen alisema kumwambia: "Hakika wewe unawaendea watu waliopewa kitabu, basi naliwe jambo la mwanzo utakalowaita kwalo ni kushuhudia kuwa hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu" na katika riwaya nyingine "Mpaka wampwekeshe Mwenyezi Mungu-, ikiwa wao watakutii katika hilo, basi wajulishe kuwa Mwenyezi Mungu amewafaradhishia juu yao swala tano katika kila usiku na mchana, ikiwa wao watakutii kwa hilo, basi wajulishe kuwa Mwenyezi Mungu amewafaradhishia juu yao sadaka, zinachukuliwa kutoka kwa matajiri wao, na kurejeshwa kwa masikini wao,ikiwa wao watakutii kwa hilo, basi tahadhari na mali zao za thamani, na ogopa sana maombi ya mwenye kudhulumiwa, kwani hayo hayana kati yake na Mwenyezi Mungu kizuizi".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Nikuwa Mtume rehema na Amani zimfikie alipomuelekeza Muadhi bin Jabali radhi za Mwenyezi Mungu zimfikie kwenda katika nchi ya Yemen kama mlinganizi (muhubiri) na Mwalimu, alimchorea mikakati ambayo atapitia katika ufikishaji wake, akamuweka wazi kuwa yeye atakutana na watu wenye elimu na mijadala miongoni mwa mayahudi na wakristo, ili awe na maandalizi ya kujadiliana nao na kujibu hoja zao, kisha aanze katika ufikishaji wake kwa jambo la Muhimu zaidi kisha linalofuata, awaite kurekebisha itikadi kwanza; kwasababu ndio msingi, wakilitii hilo awaamrishe kusimamisha swala, kwasababu ndio wajibu mkubwa baada ya Tauhidi, ikiwa wataisimamisha awaamrishe matajiri wao kutoa zaka za mali zao kuwapa mafukara wao, kwaajili ya kuwaliwaza na kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu, kisha akamtahadharisha na kutochukua mali nzuri; kwasababu ya wajibu ni ya kati na kati, kisha akamuhimiza juu ya uadilifu na kuacha dhulma; ili aliyedhulumiwa asijekumuombea dua mbaya na dua yake ni yenye kupokelewa.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Sheria ya kutuma walinganizi kwaajili ya Mwenyezi Mungu Mtukufu.
  2. Nikuwa kushuhudia kuwa hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu ndio wajibu wa kwanza na ndio la mwanzo kulinganiwa watu.
  3. Nikuwa kushuhudia kuwa hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu ni kumpwekesha Mwenyezi Mungu kwa ibada, na kuacha ya visivyokuwa yeye.
  4. Nikuwa anaweza kuwa msomi lakini asijue maana ya Laa ilaaha illa llaahu (Hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu), au akaijua na asiifanyie kazi kama ilivyo hali ya watu wa kitabu.
  5. Nikuwa kuzungumza na msomi si sawa na kuzungumza na mjinga: "hakika wewe unawaendea watu wa kitabu".
  6. Kutahadharishwa kuwa ni lazima kwa mwanadamu hususani mfikishaji awe na elimu ya dini yake; ili aepukane na utata wa wenye kutatiza, na hilo ni kwa kutafuta elimu.
  7. Nikuwa swala ndio wajibu mkubwa baada ya shahada mbili.
  8. Ulazima wa swala tano.
  9. Kuwa swala ya witiri sio wajibu.
  10. Nikuwa zaka ni nguzo ya lazima baada ya swala.
  11. Haifai kutoa zaka kuwapa matajiri.
  12. Kubainishwa mgao katika migao ya zaka, nao ni mafukara, na kufaa kuishia kuwapa wao tu, si lazima kuyaeneza makundi yote nane katika mgao wa zaka.
  13. Sheria ni kugawanywa zaka kwa watu wa kila mji kwa mafukara wao; kwa mujibu wa hadithi hii, ikiwa kuihamisha zaka kuipeleka katika mji mwingine kuna maslahi makubwa yanayopelekea hivyo, hakuna tatizo katika hilo; kama kuwa na shida kubwa katika mji mwingine, au kuwa na ndugu wa karibu ambao ni mafukara na mfano wake.
  14. Nikuwa zaka haitolewi kwa kafiri.
  15. Nikuwa haifai kuchukua mali nzuri zaidi ila kwa ridhaa ya mwenye nayo.
  16. Uharamu wa kuchukua zaka katika mali inayopendeka, bali achukue ya kati na kati.
  17. Kutahadhari na dhulma, nakuwa dua ya mwenye kudhulumiwa ni yenye kupokelewa hata kama atakuwa muovu.