عن عبد الله بن الشخير رضي الله عنه قال: "انطلقت في وفد بني عامر إلى رسول الله صلى الله عليه وسلم فقلنا: أنت سيدنا. فقال السيد الله -تبارك وتعالى-. قلنا: وأَفْضَلُنَا فَضْلًا وأَعْظَمُنْا طَوْلًا. فقال: قولوا بقولكم أو بعض قولكم، ولا يَسْتَجْرِيَنَّكُمُ الشيطان".
[صحيح] - [رواه أبو داود وأحمد]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abdillahi bin Shikh-khir -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: "Nilitoka katika kundi la Bani Aamir kwenda kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- tukasema: Wewe ni bwana wetu, basi akasema Bwana ni Mwenyezi Mungu -Aliyetakasika na kutukuka-. Tukasema: Na mbora wetu kwa fadhila na mtukufu wetu katika uwezo. Basi akasema: semeni kwa kauli zenu au baadhi ya kauli zenu, na wala asikufanyeni shetani kuwa wawakilishi wake".
Sahihi - Imepokelewa na Abuu Daud

Ufafanuzi

Lilipopitiliza na kuzidisha kundi hili katika kumsifia Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Aliwakataza kuhusu hilo; kwaajili ya kuwa na adabu na Mwenyezi Mungu -Mtukufu- na kwa kuilinda Tauhidi, na akawaamrisha waishie katika matamshi ambayo hayana kuvuka mipaka ndani yake wala makatazo, kama kumuita Muhammadi ni Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, kama alivyomuita Mwenyezi Mungu -Aliyetakasika na kutukuka-, au Nabii wa Mwenyezi Mungu, au baba Qassim, na akawatahadharisha asijekuwafanya shetani kuwa ni mawakala wake katika matendo anayowatia wasiwasi kwao.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Pashto Kiassam السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama