عن جابر بن عبد الله رضي الله عنهما أنّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم قال: «أُعْطِيتُ خمسا، لم يُعْطَهُنَّ أحد من الأنبياء قبلي: نُصِرْتُ بالرعب مسيرة شهر، وجُعِلَت لي الأرض مسجدا وطَهُورا، فأَيَّمَا رجل من أمتي أدركته الصلاة فَلْيُصَلِّ، وأُحِلَّت لي المغانم، ولم تحلَّ لأحد قبلي، وأُعْطِيتُ الشفاعة، وكان النبي يُبْعَثُ إلى قومه خاصة، وبُعِثتُ إلى الناس عامَة».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Jabiri bin Abdillah -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- yakwamba Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Nimepewa mambo matano, hajapewa yeyote katika manabii kabla yangu: nimenusuriwa (nimeepushwa) na hofu kiasi cha kutembea mwezi mzima, na imefanywa ardhi kwangu kuwa ni msikiti na ni mahala twahara (safi), Hivyo basi mtu yeyote katika umma wangu itakapomkuta swala basi na aswali, na nimehalalishiwa kwangu ngawira, na hazikuhalalishwa kwa yeyote kabla yangu, na nimepewa utetezi, na alikuwa Nabii yeyote anatumwa kwa watu wake tu, na mimi nimetumwa kwa watu wote"
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Amempendelea Mwenyezi Mungu -Mtukufu- Nabii wetu -Rehema na Amani ziwe juu yake- kuliko Manabii wengine kwa mambo matukufu, na akafanywa tofauti kwa mambo mazuri ambayo hayakuwa kwa waliokuwa kabla yake katika Manabii -Amani iwe juu yao- Ukapata umma huu kwa baraka za Nabii huyu Mtukufu na mzuri sehemu katika fadhila na ukarimu. Na miongoni mwa hayo: Ni yale yaliyothibiti katika hadithi hii katika mambo haya matano mazuri: La kwanza: Nikuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu kamnusuru, na akampa nguvu juu ya maadui zake, kwa hofu inayowapata maadui zake, ikawadhoofisha na ikasambaratisha umoja wao, hata kama atakuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- hajawafikia kwa mwendo wa kutembea mwezi mzima kutoka mahala walipo, ikiwa ni msaada toka kwa Mwenyezi Mungu na ni nusura kwa Nabii wake na nikuwavunja nguvu na kuwafelisha maadui wa dini yake, na hakuna shaka kuwa huu ni msaada mkubwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu. La pili: Nikuwa Mwenyezi Mungu -Aliyetakasika na kutukuka- Amemtanulia Nabii huyu mkarimu, na umma wake wenye kuhurumiwa kwa kuufanyia ardhi yote kuwa ni msikiti, itakaowakuta swala basi na waswali, kwani haihusiki na maeneo maalumu tu, kama ilivyokuwa kwa wale waliokuwa kabla yao walikuwa hawatekelezi ibada zao isipokuwa katika makanisa, au mahekalu, na hivi ndivyo ambavyo Mwenyezi Mungu kaondoa uzito na dhiki kwa umma huu, na akaufanya udongo kwa ambaye hakupata maji kuwa ni twahara, na mfano wake ni yule aliyeshindwa kuyatumia maji kwasababu ya madhara. La tatu: Nikuwa zile ngawira zinazochukuliwa kwa makafiri na wenye kupigana ni halali kwa Nabii -Rehema na Amani ziwe juu yake- yeye na umma wake, wanazigawana kwa mujibu wa maelekezo ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, baada yakuwa zilikuwa haramu kwa Manabii waliotangulia na umma zao, kiasi kwamba walikuwa wakizikusanya, ikiwa kama Mwenyezi Mungu kakubali amali yao basi unateremka moto toka mbinguni unaziunguza. La nne: Nikuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, kampendelea kwa kumpa nafasi nzuri, na utetezi mkuu, siku ambayo watakuwa wazito kusogea wale Mitume wakubwa katika viwanja vya kiyama, atasema mimi ndiye mwenye hilo, na atasujudu chini ya arshi, na amtukuze Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa yale yanayomstahiki, patasemwa: Omba utetezi usikilizwe, na omba upewe, hapo atamuomba Mwenyezi Mungu utetezi wa viumbe wa kuamuliwa kati yao katika kisimamo hiki kirefu, na hii ndiyo sehemu nzuri ambayo watakayomuonea wivu wa mwanzo na wa mwisho. La tano: Nikuwa kila Nabii katika Manabii waliotangulia ujumbe wao unawahusu watu wao pekee. Na ameifanya Mwenyezi Mungu Mtukufu sheria hii kuwa inafaa kwa kila zama na sehemu, na kwa kupatikana kufaa huku na ukamilifu huu, basi ukawa ndio ujumbe wa mwisho, kwasababu ni ujumbe ambao hauhitaji ziada wala hauna mapungufu ndani yake, kwa jinsi ulivyo na dondoo za kubakia na kukaa milele.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama