عن طارق بن شهاب البجلي الأحمسي رضي الله عنه أنّ رجُلًا سأل النبي صلى الله عليه وسلم وقد وضَع رِجله في الغَرْزِ: أَيُّ الجهاد أفضل؟ قال: «كَلِمَةُ حَقًّ عِند سُلطَان جَائِرٍ».
[صحيح] - [رواه النسائي وأحمد]
المزيــد ...

Kutoka kwa Twariq bin Shihabi Al bajaliy Al Ahmashiy -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Yakwamba mtu mmoja alimuuliza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- na mguu wake ukiwa tayari umeuweka kwenye kipandwa (yaani yuko tayari kwa safari): Ni jihadi ipi bora? Akasema: "Ni neno la haki kwa kiongozi muovu".
Sahihi - Imepokelewa na An-Nasaaiy

Ufafanuzi

Mtu mmoja alimuuliza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake akiwa tayari kajiandaa kwaajili ya safari: Ni jihadi ipi yenye thawabu nyingi? Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- akamueleza kuwa jihadi bora, ni yeye kumuamrisha mema kiongozi dhalimu, au amkataze maovu, jihadi haishii pekee kupigana na makafiri, bali ina daraja, na iliyotajwa ndiyo ina malipo mengi zaidi; kwasababu inahofiwa mtu kuuawa au kukamatwa kwasababu ya ujeuri na kiburi cha kiongozi na kwasababu ya uchache wa wenye kujitosa katika hilo.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Kikurdi Kireno
Kuonyesha Tarjama