عن طارق بن شهاب البجلي الأحمسي رضي الله عنه أنّ رجُلًا سأل النبي صلى الله عليه وسلم وقد وضَع رِجله في الغَرْزِ: أَيُّ الجهاد أفضل؟ قال: «كَلِمَةُ حَقًّ عِند سُلطَان جَائِرٍ».  
                        
[صحيح] - [رواه النسائي وأحمد]
                        
 المزيــد ... 
                    
Kutoka kwa Twariq bin Shihabi Al bajaliy Al Ahmashiy -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Yakwamba mtu mmoja alimuuliza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- na mguu wake ukiwa tayari umeuweka kwenye kipandwa (yaani yuko tayari kwa safari): Ni jihadi ipi bora? Akasema: "Ni neno la haki kwa kiongozi muovu". 
                                                     
                                                                                                    
[Sahihi] - [Imepokelewa na An-Nasaaiy - Imepokelewa na Ahmad]                                            
Mtu mmoja alimuuliza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake akiwa tayari kajiandaa kwaajili ya safari: Ni jihadi ipi yenye thawabu nyingi? Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- akamueleza kuwa jihadi bora, ni yeye kumuamrisha mema kiongozi dhalimu, au amkataze maovu, jihadi haishii pekee kupigana na makafiri, bali ina daraja, na iliyotajwa ndiyo ina malipo mengi zaidi; kwasababu inahofiwa mtu kuuawa au kukamatwa kwasababu ya ujeuri na kiburi cha kiongozi na kwasababu ya uchache wa wenye kujitosa katika hilo.