عن ابن مسعود رضي الله عنه أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: «ما من نبي بعثه الله في أُمَّةٍ قبلي إلا كان له من أُمَّتِهِ حَوَارِيُّونَ وأَصْحَابٌ يأخذون بسُنته ويَقْتَدُونَ بأَمره، ثم إنها تَخْلُفُ من بعدهم خُلُوفٌ يقولون ما لا يفعلون، ويفعلون ما لا يُؤْمَرُونَ، فمن جَاهَدَهُمْ بيده فهو مؤمن، ومن جَاهَدَهُمْ بقلبه فهو مؤمن، ومن جَاهَدَهُمْ بلسانه فهو مؤمن، وليس وَرَاءَ ذلك من الإيمان حَبّةُ خَرْدَلٍ».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa bin Mas'udi -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- yakwamba Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Hakuna Nabii aliyetumwa na Mwenyezi Mungu katika umma wowote kabla yangu, isipokuwa kunakuwa katika umma wake na watu wake wapendwa na watu wanaoyachukua mafundisho yake na wanafuata amri yake, kisha wanakuja kutofautiana baada yao watu wanaowafuata, wanazungumza yale wasiyoyafanya, na wanafanya ambayo hawakuamrishwa, atakayepigana nao kwa mkono wake basi huyo ndio muumini, na atakayepigana nao kwa moyo wake basi naye ni muumini, na atakayepigana nao kwa ulimi wake basi naye ni muumini, na hakuna zaidi hapo katika imani punje ndogo ya ulezi" (yaani kwa asiyefanya hivyo hana imani hata punje ndogo).
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Hakuna Nabii aliyemtuma Mwenyezi Mungu Mtukufu katika umma kabla ya Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- isipokuwa atakuwa katika umma wake na wateule na watu wa ndani wanaofaa kwa uongozi baada yake, na jamaa wanaochukua njia yake na sheria zake, na wanaiga na kutekeleza amri yake, kisha wanatokea baada yao vizazi wanajivisha yale ambayo hawakupewa, yaani wanajidhihirisha kuwa wao wako katika sifa miongoni mwa sifa njema hali yakuwa hawako hivyo, na wanafanya kinyume na yale yaliyoamrishwa katika maovu ambayo sheria haikuja nayo, atakayepigana nao kwa mkono wake; itakapolazimika kuuondoa uovu juu yake, na kukawa hakuna madhara yenye nguvu kuliko hilo basi huyo ana imani kamili, na atakayepigana nao kwa ulimi wake kwa kuwakemea na akaomba msaada kwa anayeweza kuwazuia basi naye ni muumini, na atakayepigana nao kwa moyo wake, na akataka msaada katika kuuondoa uovu huo kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu basi naye ni muumini, na hakuna nyuma ya kuuchukia uovu kwa moyo katika imani chochote (yaani, zaidi ya hapo mtu atakuwa hana imani hata punje ndogo).

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama