عن أبي هريرة رضي الله عنه أَنَّهُ سَمِعَ النَّبيَّ -صلّى اللهُ عليه وسَلَّم يقول-: «إن العبد ليتكلم بالكلمة ما يتبين فيها يزلُّ بها إلى النار أبعدَ مما بين المشرق والمغرب».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake-yakwamba yeye alimsikia Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- akisema:"Hakika mja anaweza kuzungumza neno,asilijali ndani yake akateleza kwa neno hilo na kuingia katika moto ambao umbali wake ni baina ya mashariki na magharibi".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Anatueleza sisi Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kuwa kuna baadhi ya watu huwa hawafikirii wanapotaka kuzungumza, je maneno haya nitakayoyazungumza ni ya kheri au la?. na matokeo yanakuwa huyu mzungumzaji anatumbukia kwasababu ya kutofikiria mambo ya haramu, na anaitia nafsi yake katika adhabu ya Mwenyezi Mungu katika moto wa jahanamu, -Mwenyezi Mungu atukinge- na huenda akaporomoka katika moto masafa marefu umbali wa masafa kati ya mashariki na magharibi.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Kikurdi Kireno Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri
Kuonyesha Tarjama