+ -

عن أبي هريرة رضي الله عنه أَنَّهُ سَمِعَ النَّبيَّ -صلّى اللهُ عليه وسَلَّم يقول-: «إن العبد ليتكلم بالكلمة ما يتبين فيها يزلُّ بها إلى النار أبعدَ مما بين المشرق والمغرب».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake-yakwamba yeye alimsikia Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- akisema:"Hakika mja anaweza kuzungumza neno,asilijali ndani yake akateleza kwa neno hilo na kuingia katika moto ambao umbali wake ni baina ya mashariki na magharibi".
[Sahihi] - [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim]

Ufafanuzi

Anatueleza sisi Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kuwa kuna baadhi ya watu huwa hawafikirii wanapotaka kuzungumza, je maneno haya nitakayoyazungumza ni ya kheri au la?. na matokeo yanakuwa huyu mzungumzaji anatumbukia kwasababu ya kutofikiria mambo ya haramu, na anaitia nafsi yake katika adhabu ya Mwenyezi Mungu katika moto wa jahanamu, -Mwenyezi Mungu atukinge- na huenda akaporomoka katika moto masafa marefu umbali wa masafa kati ya mashariki na magharibi.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kireno Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri
Kuonyesha Tarjama