عن أبي هريرة رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم قال: «أتدرون ما الغِيبَةُ؟»، قالوا: الله ورسوله أعلم، قال: «ذكرُك أخاك بما يكره»، قيل: أرأيت إن كان في أخي ما أقول؟ قال: «إن كان فيه ما تقول فقد اغْتَبْتَهُ، وإن لم يكن فقد بَهَتَّهُ».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Huraira Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake Amesema: "Je mnajua ni nini kusengenya?" wakasema: Mwenyezi Mungu na Mtume wake ndio wajuzi, akasema: "Ni kumsema kwako ndugu yako kwa yale anayoyachukia" pakasemwa: Unasemaje yakiwa kwa ndugu yangu haya ninayoyasema? Akasema: "Akiwanayo hayo unayoyasema utakuwa umemsengenya, na akiwa hana basi utakuwa umemzulia uongo".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim
Amebainisha Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake maana halisi ya kusengenya, Nayo ni: kumsema muislamu asiyekuwepo kwa yale anayoyachukia, sawa sawa iwe ni katika sifa zake za kimaumbile au za kitabia hata kama sifa hizo atakuwa nazo, na ikiwa kama atakuwa hana sifa hizo basi utakuwa umekusanya pamoja na kusengenya sifa uongo na uzushi kwa mtu asiyekuwa nazo.