عن أم سلمة هند بنت أبي أمية حذيفة رضي الله عنها عن النبي صلى الله عليه وسلم أنه قال: «إِنَّه يُسْتَعمل عَلَيكُم أُمَرَاء فَتَعْرِفُون وَتُنكِرُون، فَمَن كَرِه فَقَد بَرِئ، ومَن أَنْكَرَ فَقَد سَلِمَ، ولَكِن مَنْ رَضِيَ وَتَابَعَ» قالوا: يا رسول الله، أَلاَ نُقَاتِلُهُم؟ قال: «لا، ما أَقَامُوا فِيكُم الصَّلاَة».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Ummu Salama Hindu binti Abii Umaiyya Hudhaifa- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Kutoka kwa Mtume Rehema na Amani zimfikie- Yakwamba yeye amesema: "Hakika watakuongozeni nyinyi viongozi ambao watafanya mambo mtayajua na mengine hamtoyajua, atakayechukia atakuwa kajiepusha, na atakayepinga atakuwa kasalimika, lakini atakaye ridhia na akafuatisha", wakasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, kwanini tusiwapige vita? Akasema: "Hapana, madam bado wanasimamisha kwenu nyinyi swala".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Ameeleza -ziwe juu yake sala na salamu- kuwa watateuliwa juu yetu sisi kutoka kwa kiongozi mkuu, viongozi ambao tutafahamu baadhi ya matendo yao; kwa kuendana kwake na yale yanayojulikana katika sheria, na tutayapinga baadhi yake, kwa kwenda kwake kinyume na hilo, atakayeuchukia uovu kwa moyo wake na akawa hakuweza kuukemea; kwa kuogopa nguvu zao basi atakuwa ameepukana na madhambi, na atakayeweza kukemea kwa mkono au ulimi akawakemea, huyo basi atakuwa amesalimika, lakini atakaye ridhia vitendo vyao kwa moyo wake, na akawafuata katika kuvifanyia kazi ataangamia kama walivyoangamia. kisha wakamuuliza Mtume Rehema na Amani zimfikie:- kwanini tusiwapige vita? Akasema: "Hapana, Madam bado wanasimamisha kwenu nyinyi swala".

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Katika miujiza ya Mtume rehema na Amani zimfikie ni kueleza kwake yale yatakayotokea katika mambo ya ghaibu (yaliyofichikana).
  2. Katika hadithi hii: kuna ushahidi juu ya ulazima wa kukemea uovu kulingana na uwezo, na haifai kujitoa kwa viongozi, ispokuwa wakiacha swala; kwasababu ndio kitenganishi kati ya ukafiri na uislamu.
  3. kipimo katika kuondoa uovu na kumuondoa mtawala, nacho ni sheria na sio matamanio au maasi au vikundi.
  4. Haitakiwi kushirikiana na madhalimu, au kuwasaidia, au kuwa na furaha wakati wa kuwaona, na kukaa kwao pasina kuwa na haja ya kisheria.
  5. Watakapozua viongozi mambo yanayokwenda kinyume na sheria; haitakiwi kwa umma kukubaliana nao juu ya hilo.
  6. Tahadhari ya kuto chochea fitina, na kuusambaza umoja, na kuzingatiwa hilo kuwa ni ovu mno kuliko hata kuvumilia uovu wa viongozi waasi, na kuvumilia juu ya maudhi yao.
  7. Swala ndio anwani ya uislamu na ndio kitenganishi kati ya ukafiri na uislamu.
  8. Na katika hadithi hii kuna ushahidi kuwa kuacha swala ni ukafiri; na hilo ni kwasababu haifai kuwapiga vita viongozi ila kama tutaona ukafiri wa wazi ambao sisi tuna hoja kutoka kwa Mwenyezi Mungu, anapotuidhinisha sisi Mtume rehema na Amani zimfikie kuwapiga watakapokuwa hawakusimamisha swala, hilo linaonyesha kuwa kuacha swala ni ukafiri wa wazi ambao sisi tunayo hoja kutoka kwa Mwenyezi Mungu.