عن أم سلمة هند بنت أبي أمية حذيفة رضي الله عنها عن النبي صلى الله عليه وسلم أنه قال: «إِنَّه يُسْتَعمل عَلَيكُم أُمَرَاء فَتَعْرِفُون وَتُنكِرُون، فَمَن كَرِه فَقَد بَرِئ، ومَن أَنْكَرَ فَقَد سَلِمَ، ولَكِن مَنْ رَضِيَ وَتَابَعَ» قالوا: يا رسول الله، أَلاَ نُقَاتِلُهُم؟ قال: «لا، ما أَقَامُوا فِيكُم الصَّلاَة».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...
Kutoka kwa Ummu Salama Hindu binti Abii Umaiyya Hudhaifa- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Kutoka kwa Mtume Rehema na Amani zimfikie- Yakwamba yeye amesema: "Hakika watakuongozeni nyinyi viongozi ambao watafanya mambo mtayajua na mengine hamtoyajua, atakayechukia atakuwa kajiepusha, na atakayepinga atakuwa kasalimika, lakini atakaye ridhia na akafuatisha", wakasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, kwanini tusiwapige vita? Akasema: "Hapana, madam bado wanasimamisha kwenu nyinyi swala".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim
Ameeleza -ziwe juu yake sala na salamu- kuwa watateuliwa juu yetu sisi kutoka kwa kiongozi mkuu, viongozi ambao tutafahamu baadhi ya matendo yao; kwa kuendana kwake na yale yanayojulikana katika sheria, na tutayapinga baadhi yake, kwa kwenda kwake kinyume na hilo, atakayeuchukia uovu kwa moyo wake na akawa hakuweza kuukemea; kwa kuogopa nguvu zao basi atakuwa ameepukana na madhambi, na atakayeweza kukemea kwa mkono au ulimi akawakemea, huyo basi atakuwa amesalimika, lakini atakaye ridhia vitendo vyao kwa moyo wake, na akawafuata katika kuvifanyia kazi ataangamia kama walivyoangamia. kisha wakamuuliza Mtume Rehema na Amani zimfikie:- kwanini tusiwapige vita? Akasema: "Hapana, Madam bado wanasimamisha kwenu nyinyi swala".