عن معقل بن يسار رضي الله عنه مرفوعاً: «ما من عبد يَسْتَرْعِيْهِ الله رَعِيَّةً، يموت يوم يموت، وهو غاشٌّ لِرَعِيَّتِهِ؛ إلا حرَّم الله عليه الجنة».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Ma'qili bin Yasari Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Hakuna mja yeyote atakayempa Mwenyezi Mungu raia, akafa siku anakufa, haliyakuwa aliwafanyia ghushi (udanganyifu) ispokuwa atamharamishia Mwenyezi Mungu pepo".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Katika hadithi ya Ma'qil bin Yasari hii kuna tahadhari ya kuwafanyia raia udanganyifu, nakuwa: (Hakuna mja yeyote atakayempa Mwenyezi Mungu raia): Yaani akampatia usimamizi wa kuwaongoza raia: nayo inamaana ya wenye kuongozwa, kwa kumuweka kusimamia maslahi yao na akampa kushika hatamu ya mambo yao, na msimamizi: Ni mwangalizi aliyeaminiwa juu ya yale yanayowaelekea raia nayo ni utunzaji. (Akafa siku anakufa haliyakuwa amewafanyia udanganyifu) Yaani hiyana (kwa raia wake) makusudio ya siku anakufa ni wakati wa kutoka roho yake, na hali zilizo kabla yake haikubaliki ndani yake toba; kwasababu mwenye kutubia kutokana na hiyana yake au uzembe wake hastahiki ahadi hii. Itakayejitokeza hiyana katika uongozi wake, sawa sawa uwe uongozi ni wa kuongoza umma, au maalumu; basi hakika mkweli mwenye kusadikishwa ziwe juu yake sala bora na salama tukufu kamuahidi kwa kauli yake: (Ispokuwa Mwenyezi Mungu atamharamishia pepo) Yaani ikiwa atalihalalisha hilo (dhambi lake) au makusudio yake atamzuia kuingia kwake peponi na wale wa mwanzo.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Ahadi kali kwa viongozi ambao hawajali mambo ya raia wao.
  2. Hadithi hii si maalumu kwa kiongozi mkuu tu na naibu wake, bali inamjumlisha kila ambaye Mwenyezi Mungu atampa usimamizi wa raia, kama baba na mwalimu mkuu wa shule na mfano wake.
  3. Nikuwa ikiwa atatubia huyu mdanganyifu kabla ya kifo chake haitompata ahadi hii.
  4. Tahadhari kwa mahakimu kutokana na kutofanya uzembe juu ya haki za raia wao na kupuuza kesi zao na kupoteza haki zao.
  5. Kubainishwa wajibu wa mahakimu katika kuhakikisha wanatumia juhudi zao za mwisho kuwanasihi raia wao, nakuwa atakayefanya uzembe katika hilo ataharamishiwa pepo pamoja na wale waliofaulu.
  6. Kubainishwa umuhimu wa cheo cha uhakimu katika uislamu.