عن عرفجة رضي الله عنه قال: سمعت رسول الله صلى الله عليه وسلم يقول: "من أتاكم وأمرُكُم جَمِيْعٌ على رجل واحد، يُريد أن يَشُقَّ عَصَاكُم، أو يُفَرِّقَ جَمَاَعَتَكُم، فاقتُلُوهُ".
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...
Kutoka kwa A'rfaja -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Nilimsikia Mumbe wa Mwenyezi Mungu Rehema na Amani ziwe juu yake akisema: "Yeyote Atakayekujieni na akakuamrisheni nyote muwe dhidi ya mtu mmoja, akataka kupasua nguvu yenu, na usambaratishe umoja wenu, basi muuweni".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim
Lengo la hadithi hii ni katika kupambana na watu waovu, na anayetaka kusambaratisha umoja wa waislamu baada kukusanyika kwao na kumtii kwao kiongozi, na imeonyesha kuwa waislamu wakikubaliana juu ya kiongozi mmoja, kisha akaja anayetaka kumuondoa kiongozi wao ambaye wao wamekubaliana juu yake, ni wajibu kwao wamsimamishie sheria hata kama ni kwa kumuua; kwaajili ya kuzuia shari zake na kulinda damu za waislamu.