عن أبي هريرة رضي الله عنه مرفوعًا: «والذي نفسُ مُحمَّد بيدِه، لا يسمعُ بي أحدٌ من هذه الأمة يهوديٌّ، ولا نصرانيٌّ، ثم يموتُ ولم يؤمن بالذي أُرْسِلتُ به، إلَّا كان مِن أصحاب النار».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u-: "Namuapa yule ambaye nafsi ya Muhammadi iko mkononi mwake, hatonisikia yeyote katika umma huu, Myahudi wala Mkristo, kisha akafa haliyakuwa hajayaamini yale niliyotumwa kwayo, ispokuwa atakuwa ni katika watu wa motoni".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Anaapa Mtume rehema na Amani zimfikie kwa Mwenyezi Mungu yakuwa yeye: "hatomsikia katika umma huu" Yaani: kwa wale waliopo katika zama zake na baada yake mpaka siku ya kiyama "Myahudi wala mkristo, kisha akafa, na akawa hakuyaamini yale niliyotumwa kwayo, ispokuwa atakuwa katika watu wa motoni" Myahudi yeyote au mkristo yeyote au wengineo utakayemfikia ujumbe wa Mtume rehema na Amani zimfikie kisha akafa na hajamuamini ispokuwa atakuwa katika watu wa motoni watakao kaa humo milele. Na bila shaka kawataja Mayahudi na Wakristo ili kuwazindua wengine, na hii ni kwasababu mayahudi na wakristo wao wana vitabu, ikiwa hii ndiyo hali yao pamoja nakuwa wao wana vitabu, hivyo wengine wasiokuwa na vitabu ndiyo zaidi, wote hao wanalazimika kuingia katika dini yake na kumtii yeye rehema na Amani ziwe juu yake.

Kufanya Tarjama: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibaghali Kichina Kifursi Kihindi Kisin-hala Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese German Kijapani
Kuonyesha Tarjama

Faida nyingi

  1. Na ambaye hatomsikia Mtume rehema na Amani zimfikie na ukawa haujamfikia ujumbe wa Uislamu basi huyu atapewa udhuru.
  2. Ulazima wa kumfuata yeye rehema na Amani zimfikie, na kufuta sheria zote kwa sheria yake, atakayemkufuru haitomsaidia yeye imani yake ya kuwaamini Manabii wengine sala na salamu za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao wote.
  3. Kunufaika na uislamu muda kidogo kabla ya kifo, hata kama itakuwa ni wakati wa maradhi sana, madam tu hali haijafikia katika umauti (sakaratil mauti).
  4. Kumkufurisha mwenye kupinga baadhi ya yale aliyokuja nayo Mtume rehema na Amani ziwe juu yake, litakapothibiti hilo kwa ushahidi wa wazi, na umma ukawa umekubaliana.