عن أبي هريرة رضي الله عنه مرفوعاً: «كل أمتي يدخلون الجنة إلا من أَبَى». قيل: ومَنْ يَأْبَى يا رسول الله؟ قال: «من أطاعني دخل الجنة، ومن عصاني فقد أَبَى».
[صحيح] - [رواه البخاري]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Huraira Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Umma wangu wote utaingia peponi ispokua atakaye kataa, akaulizwa ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu ni nani atakaye kataa? akajibu: Mwenye kunitii ataingia peponi na mwenye kuniasi atakuwa amekataa".
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy
Anasimulia Abuu Huraira Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake yakwamba Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake ameupa habari njema umma wake akasema: "Umma wangu wote wataingia peponi" Yaani umma uliokubali, kisha akaondoa Ziwe juu yake sala na salamu akasema: "Ispokuwa atakayekataa" Yaani: Atakaye asi miongoni mwao akaacha utiifu ambao ni sababu ya kuingia peponi; kwasababu atakayeacha mambo ambayo ndiyo sababu ya kitu fulani na hakipatikani kwasababu nyingine huyo atakuwa kakataa yaani amejizuilia; kujivua kwao ni sababu ya kutiwa uzito jambo lao juu yao, Au alikusudia Umma wa kufikishiwa: Na atakayekataa kwa kupinga kwa kukataa kwake kukubali. wakasema maswahaba watukufu:"Na ni nani atakayekataa ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu?" Akawajibu ziwe juu yake sala na salamu: "Atakaye nitii mimi" Yaani akatii na akakubali yale niliyokuja nayo "Ataingia peponi". Na ama "atakayeniasi" baada ya kuamini au kwa kufanya makatazo "Atakuwa kakataa": Atakuwa na marejeo mabaya kwa kukataa kwake. Na ni juu yake: Atakayekataa akiwa kama ni kafiri hatoingia peponi kabisa, na ama atakayekuwa ni muislamu basi yeye hatoiingia mpaka asafishwe kwa moto, na unaweza kumfikia msamaha asiadhibiwe kabisa hata kama alifanya maasi yote.