عن أبي عبد الله جابر بن عبد الله الأنصاري رضي الله عنهما أن رجلاً سأل رسول الله صلى الله عليه وسلم فقال: أرأيت إذا صليت المكتوبات، وصمت رمضان، وأحللت الحلال، وحرمت الحرام، ولم أزد على ذلك شيئاً، أأدخل الجنة؟ قال: «نعم».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Abdillahi Jabiri bin Abdillahi Al Answari Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao, yakwamba mtu mmoja alimuuliza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- akasema: Unaonaje kama nitaswali swala za faradhi, na nikafunga ramadhani, na nikahalalisha halali na nikaharamisha haramu, na nikawa sikuzidisha zaidi ya hapo chochote, Je, naweza kuingia peponi? Akasema: "Ndiyo".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Amepokea Abuu Abdillahi Jabiri bin Abdillahi Al Answari Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao, yakwamba mtu mmoja alimuuliza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- Akasema: Unaonaje: Yaani: Nieleze ikiwa nitaswali swala za faradhi, yaani swala tano za lazima, na nikawa sikuzidisha juu yake swala za sunna, na nikafunga ramadhani pekee bila kuongeza funga za sunna, na nikahalalisha halali, yaani nikafanya yale ya halali pamoja na kuharamisha haramu, yaani nikajiepusha na nikajiweka mbali nikiamini uharamu wake, nikatosheka na halali pekee, na nikawa sikuzidisha zaidi ya hapo chochote, Je, hilo linaweza kutosha kuingia peponi? Akajibu Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- (Ndiyo), kwasababu maana ya uchamungu ni kufanya maamrisho na kuacha makatazo, na mtu wa namna hii ndiye anayejulikana katika maandiko kuwa ni (Muqtaswid) aliyetosheka, naye ni yule asiyezidisha katika yale aliyomuwajibishia Mwenyezi Mungu juu yake, na haachi zaidi ya yale aliyoyaharamisha Mwenyezi Mungu juu yake.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Pupa ya maswahaba katika kutaka kuijua haki na uongofu na kushikamana nayo, na pupa yao ya kutaka kujua yale yenye kufikisha peponi na yanayoweza kuwafikisha watu wa peponi.
  2. Hadithi inaonyesha kuwa pepo ndiyo lengo kuu, nakuwa mtu anafanya matendo mema ili apate radhi za Mwenyezi Mungu Mtukufu ili akampe makazi peponi kwake.
  3. Hadithi inaonyesha kuwa matendo ni sababu ya kuingia peponi.
  4. Utukufu wa swala tano, nakuwa yenyewe ndiyo amali muhimu zaidi, na ni amali kubwa zaidi baada ya shahada mbili.
  5. Ukubwa wa swala la kufunga ramadhani, na huenda muulizaji alipouliza zilikuwa sheria zingine hazijakamilika, au hakuwa na mali ya kuweza kutoa zaka.
  6. Nikuwa mwanadamu anatakiwa kuwa mtu wa kufuata na kuendana na yale yaliyokuja kutoka kwa Mwenyezi Mungu na kwa Mtume wake -Rehema na Amani ziwe juu yake- katika kuhalalisha halali na kuharamisha haramu, afanye yale yaliyoruhusiwa kwake miongoni mwa yale aliyoyahalalisha Mwenyezi Mungu, na ajiepushe na yale aliyoyaharamisha Mwenyezi Mungu juu yake katika yale ambayo limekuja zuio lake na katazo lake, linajumuishwa katika hayo kila lililoharamishwa pamoja na kuamini kuwa jambo hilo ni haramu.