عن ابن مسعود رضي الله عنه قال: قال النبي صلى الله عليه وسلم : «الجنة أقرب إلى أحدكُم من شِرَاكِ نَعْلِه، والنار مِثلُ ذلك».
[صحيح] - [رواه البخاري]
المزيــد ...

Kutoka kwa Ibn Mas'udi Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Amesema Mtume Rehema na Amani zimfikie-: "Pepo iko karibu na mmoja wenu kuliko hata kisigino cha kiatu chake, na moto mfano huo huo".
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy

Ufafanuzi

Anaeleza Mtume Rehema na Amani zimfikie kuwa pepo na moto viko karibu na mtu kama ukaribu wa mwendo unaokuwa juu ya kisigino, nao uko karibu mno na mtu; kwasababu yeye anaweza kufanya jambo katika yale ya kumtii Mwenyezi Mungu na kutaka radhi zake asidhanie kuwa linaweza kufikia kiwango lilichofikia, ghafla linamfikisha katika pepo yenye neema, Na yawezekana anaweza kufanya maasi na asiyachukulie uzito, nayo ni katika mambo yanayomchukiza Mwenyezi Mungu akaporomoka nayo katika moto kadhaa wa kadhaa miaka hali yakuwa yeye hajui.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Utiifu unamfikisha mtu peponi, na maasi yanapelekea kuingia motoni.
  2. Kuipata pepo ni rahisi, lengo litakapokuwa sahihi na ukafanya mema.
  3. Utiifu na maasi vinaweza kuwa katika vitu vyepesi vyepesi, hivyo inatakiwa mtu asivipuuze vitu vidogo katika kheri avifanye, wala vidogo katika shari aviepuke.
  4. Kuhimizwa katika kheri ndogo hata kama itakuwa chache, na kutishwa juu ya shari ndogo hata kama itakuwa chache.
  5. Kupigwa mifano kwaajili ya kusogeza karibu kusudio kwa msikilizaji.