عن ابن مسعود رضي الله عنه قال: قال النبي صلى الله عليه وسلم : «الجنة أقرب إلى أحدكُم من شِرَاكِ نَعْلِه، والنار مِثلُ ذلك».
[صحيح] - [رواه البخاري]
المزيــد ...
Kutoka kwa Ibn Mas'udi Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Amesema Mtume Rehema na Amani zimfikie-: "Pepo iko karibu na mmoja wenu kuliko hata kisigino cha kiatu chake, na moto mfano huo huo".
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy
Anaeleza Mtume Rehema na Amani zimfikie kuwa pepo na moto viko karibu na mtu kama ukaribu wa mwendo unaokuwa juu ya kisigino, nao uko karibu mno na mtu; kwasababu yeye anaweza kufanya jambo katika yale ya kumtii Mwenyezi Mungu na kutaka radhi zake asidhanie kuwa linaweza kufikia kiwango lilichofikia, ghafla linamfikisha katika pepo yenye neema, Na yawezekana anaweza kufanya maasi na asiyachukulie uzito, nayo ni katika mambo yanayomchukiza Mwenyezi Mungu akaporomoka nayo katika moto kadhaa wa kadhaa miaka hali yakuwa yeye hajui.