وعن جابر رضي الله عنه قال: سُئِل رسول الله صلى الله عليه وسلم أي الصلاة أفضل؟ قال: «طُول القُنُوتِ».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...
Na kutoka kwa Jabiri -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Aliulizwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake-: Ni swala ipi bora? Akasema: "Ni kurefusha kisimamo".
[Sahihi] - [Imepokelewa na Imamu Muslim]
Walimuuliza maswahaba Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- : Ni swala ipi bora? Na swali hili ni kwasababu ya pupa yao ya kuhakikisha wanapata kiwango kikubwa cha mema,Na makusudio yake:Ni aina ipi ya swala zote ndio bora? Au: Yaani ni tendo lipi katika matendo ya swala ndio bora? Ni kusimama au kurukuu au kusujudu? Akaeleza Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake kuwa ni kurefusha kisimamo ndani yake.
Kuonyesha Tarjama