وعن جابر رضي الله عنه قال: سُئِل رسول الله صلى الله عليه وسلم أي الصلاة أفضل؟ قال: «طُول القُنُوتِ».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Na kutoka kwa Jabiri -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Aliulizwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake-: Ni swala ipi bora? Akasema: "Ni kurefusha kisimamo".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Walimuuliza maswahaba Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- : Ni swala ipi bora? Na swali hili ni kwasababu ya pupa yao ya kuhakikisha wanapata kiwango kikubwa cha mema,Na makusudio yake:Ni aina ipi ya swala zote ndio bora? Au: Yaani ni tendo lipi katika matendo ya swala ndio bora? Ni kusimama au kurukuu au kusujudu? Akaeleza Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake kuwa ni kurefusha kisimamo ndani yake.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama