عن أبي هريرة رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم قال: «أَثقَل الصَّلاةِ على المُنَافِقِين: صَلاَة العِشَاء، وصَلاَة الفَجر، وَلَو يَعلَمُون مَا فِيها لَأَتَوهُمَا وَلَو حَبْوُا، وَلَقَد هَمَمتُ أًن آمُرَ بِالصَّلاَةِ فَتُقَام، ثُمَّ آمُر رجلاً فيصلي بالنَّاس، ثُمَّ أَنطَلِق مَعِي بِرِجَال معهُم حُزَمٌ مِن حَطَب إلى قَومٍ لاَ يَشهَدُون الصَّلاَة، فَأُحَرِّقَ عَلَيهِم بُيُوتَهُم بالنَّار».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Kutoka kwa Mtume rehema na Amani zimfikie Amesema: "Swala nzito juu ya wanafiki: ni swala ya ishaa na swala ya Alfajiri, na lau wangejua yaliyomo ndani ya swala hizo, basi wangeziendea hata kwa kutambaa, na nilitamani niamrishe swala ikimiwe, kisha nimuamrishe mtu awaswalishe watu, kisha niondoke wakiwa pamoja nami wanaume wakiwa na vijinga vya moto twende kwa watu ambao hawahudhurii swala nikazichome nyumba zao kwa moto".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Hakika walikuwa wanafiki wakijionyesha kwa watu, na wala hawamtaji Mwenyezi Mungu ila kidogo, kama alivyowaelezea Mwenyezi Mungu Mtukufu, na unadhihiri uvivu wao katika swala ya ishaa na swala ya Alfajiri; kwasababu ni swala ambazo ziko nyakati za giza, hivyo watu wenye kuswali hawawaoni; kwasababu takribani wanafki wote tunawaona hufanya uzembe katika swala hizi mbili ambazo ziko nyakati za kupumzika na kustareheka kwa usingizi, na hapati uchangamfu wa kuzitekeleza ila yule mwenye kusukumwa na msukumo wa imani ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, na akataraji malipo ya Akhera, na swala lilipokuwa kama ilivyoelezwa zikawa swala hizi mbili ni ngumu na nzito juu ya wanafiki, na lau wangejua yaliyomo ndani ya swala hizi kwa kuswali pamoja na waumini katika msikiti, katika malipo na thawabu basi wangeziendea hata kwa kutambaa kama mtoto kwa mikono na magoti, na akaapa rehema na Amani zimfikie - kuwa yeye hakika alitamani kuwaadhibu wenye kwenda kinyume wanaofanya uzembe kuzitekeleza pamoja na jamaa, na hilo ni aamrishe swala ikimiwe kwa jamaa, kisha amuamrishe mtu awaswalishe watu badala yake, kisha aondoke akiwa pamoja na watu wakiwa wamebeba vijinga vya moto kwenda kwa watu wasiyohudhuria swala, ili azichome nyumba zao kwa moto; kwa ubaya wa yale waliyoyafanya kwa kwenda kinyume katika swala ya jamaa, lau kusingekuwa katika majumba na wanawake na watoto wasiyokuwa na hatia, wasiyokuwa na makosa, kama ilivyokuja katika baadhi ya njia za hadithi.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Swala ya jamaa ni faradhi ya lazima, kwa wanaume waliobaleghe.
  2. Kuondoa madhara hutangulia kabla ya kuleta manufaa; kwasababu yeye hakikumzuia kuwaadhibu kwa njia hii ispokuwa ni kuhofia kumuadhibu asiyestahiki kuadhibiwa.
  3. Madhara yakiwa makubwa zaidi kuliko kukemea, basi atosheke tu kwa kukemea kuliko kufikia kuadhibu; kwa kutanguliza Mtume rehema na Amani zimfikie kitisho kabla ya adhabu.
  4. Uzito wa swala zote kwa wanafiki, nakuwa nzito zaidi ni swala mbili, ishaa na Alfajiri.
  5. Wanafiki hawakutaka kwa ibada zao ila kujionyesha na kusikika, kwasababu wao huja kuswali pale watu wanapowaona.
  6. Ubora wa swala mbili, Ishaa na Alfajiri.
  7. Ukubwa wa malipo katika swala mbili, Ishaa na Alfajiri pamoja na jamaa, nakuwa kuna haja zaidi ya kuziendea hata kwa kutambaa.
  8. Uzito wa swala mbili Ishaa na Alfajiri: unazingatiwa katika kuzitekeleza katika jamaa, na hii ndio maana inayoonyeshwa na mlolongo wa maneno, bali zimekuwa nzito zaidi kwa msukumo mkubwa uliyoko (ndani ya moyo) wa kwenda kinyume nazo, na nguvu kubwa ya kujiepusha kuzihudhuria.
  9. Imamu inapojitokeza kwake shughuli basi aache badala yake wa kuwaswalisha watu.
  10. Kuwachukulia waovu ukali.