عن أبي هريرة رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم قال: «أَثقَل الصَّلاةِ على المُنَافِقِين: صَلاَة العِشَاء، وصَلاَة الفَجر، وَلَو يَعلَمُون مَا فِيها لَأَتَوهُمَا وَلَو حَبْوُا، وَلَقَد هَمَمتُ أًن آمُرَ بِالصَّلاَةِ فَتُقَام، ثُمَّ آمُر رجلاً فيصلي بالنَّاس، ثُمَّ أَنطَلِق مَعِي بِرِجَال معهُم حُزَمٌ مِن حَطَب إلى قَومٍ لاَ يَشهَدُون الصَّلاَة، فَأُحَرِّقَ عَلَيهِم بُيُوتَهُم بالنَّار».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Huraira radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Kutoka kwa Mtume rehema na Amani zimfikie Amesema: "Swala nzito juu ya wanafiki: ni swala ya ishaa na swala ya Alfajiri, na lau wangejua yaliyomo ndani ya swala hizo, basi wangeziendea hata kwa kutambaa, na nilitamani niamrishe swala ikimiwe, kisha nimuamrishe mtu awaswalishe watu, kisha niondoke wakiwa pamoja nami wanaume wakiwa na vijinga vya moto twende kwa watu ambao hawahudhurii swala nikazichome nyumba zao kwa moto".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim
Hakika walikuwa wanafiki wakijionyesha kwa watu, na wala hawamtaji Mwenyezi Mungu ila kidogo, kama alivyowaelezea Mwenyezi Mungu Mtukufu, na unadhihiri uvivu wao katika swala ya ishaa na swala ya Alfajiri; kwasababu ni swala ambazo ziko nyakati za giza, hivyo watu wenye kuswali hawawaoni; kwasababu takribani wanafki wote tunawaona hufanya uzembe katika swala hizi mbili ambazo ziko nyakati za kupumzika na kustareheka kwa usingizi, na hapati uchangamfu wa kuzitekeleza ila yule mwenye kusukumwa na msukumo wa imani ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, na akataraji malipo ya Akhera, na swala lilipokuwa kama ilivyoelezwa zikawa swala hizi mbili ni ngumu na nzito juu ya wanafiki, na lau wangejua yaliyomo ndani ya swala hizi kwa kuswali pamoja na waumini katika msikiti, katika malipo na thawabu basi wangeziendea hata kwa kutambaa kama mtoto kwa mikono na magoti, na akaapa rehema na Amani zimfikie - kuwa yeye hakika alitamani kuwaadhibu wenye kwenda kinyume wanaofanya uzembe kuzitekeleza pamoja na jamaa, na hilo ni aamrishe swala ikimiwe kwa jamaa, kisha amuamrishe mtu awaswalishe watu badala yake, kisha aondoke akiwa pamoja na watu wakiwa wamebeba vijinga vya moto kwenda kwa watu wasiyohudhuria swala, ili azichome nyumba zao kwa moto; kwa ubaya wa yale waliyoyafanya kwa kwenda kinyume katika swala ya jamaa, lau kusingekuwa katika majumba na wanawake na watoto wasiyokuwa na hatia, wasiyokuwa na makosa, kama ilivyokuja katika baadhi ya njia za hadithi.