عن عائشة رضي الله عنها : أن النبي صلى الله عليه وسلم كان يصلي صلاته بالليل، وهي مُعْتَرِضَةٌ بين يديه، فإذا بقي الوتر، أيقظها فأوترت. وفي رواية له: فإذا بقي الوتر، قال: «قومي فأوْتِري يا عائشة».
[صحيح] - [متفق عليه ولفظ الروايتين لمسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Aisha -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Yakwamba Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- alikuwa akiswali swala zake za usiku, naye akiwa kajilaza mbele yake, inapobakia witiri, anamuamsha na anaswali witiri. Na katika riwaya yake: inapobakia witiri, anasema: "Simama na uswali witiri ewe Aisha".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Maana ya hadithi: Nikuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- alikuwa akiswali swala za usiku, na Aisha -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- akiwa kajilaza mbele yake, na katika riwaya ya Bukhariy na Muslim kutoka kwake: "Nikuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- alikuwa akiswali usiku na mimi nikiwa nimejilaza kati yake na kibla, kama linavyolazwa jeneza". Anapomaliza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- swala ya usiku (tahajjudi), na kabla hajaanza swala ya witiri anamuamsha kwaajili ya witiri, na katika riwaya ya Muslim: Inapobakia witiri, anasema: "Simama na uswali witiri ewe Aisha". Na katika riwaya ya Abiidaudi: "Mpaka anapotaka kuswali witiri basi anamuamsha na anaswali witiri". Na maana yake: Nikuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- alikuwa akimuacha Aisha -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- mwanzo wa usiku wala hamuamshi, mpaka anapomaliza swala zake na ikawa haijabakia isipokuwa witiri anamuamsha ili naye apate witiri yake, na afanye haraka kuswali witiri baada ya kuamka ili uvivu wa usingizi usimzidie, lau kama akimzembea ikampita.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kireno
Kuonyesha Tarjama