عَنْ أُبَيِّ بْنِ كَعْبٍ رَضيَ اللهُ عنه قَالَ:
كَانَ رَجُلٌ لَا أَعْلَمُ رَجُلًا أَبْعَدَ مِنَ الْمَسْجِدِ مِنْهُ، وَكَانَ لَا تُخْطِئُهُ صَلَاةٌ، قَالَ: فَقِيلَ لَهُ: أَوْ قُلْتُ لَهُ: لَوْ اشْتَرَيْتَ حِمَارًا تَرْكَبُهُ فِي الظَّلْمَاءِ، وَفِي الرَّمْضَاءِ، قَالَ: مَا يَسُرُّنِي أَنَّ مَنْزِلِي إِلَى جَنْبِ الْمَسْجِدِ، إِنِّي أُرِيدُ أَنْ يُكْتَبَ لِي مَمْشَايَ إِلَى الْمَسْجِدِ، وَرُجُوعِي إِذَا رَجَعْتُ إِلَى أَهْلِي، فَقَالَ رَسُولُ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: «قَدْ جَمَعَ اللهُ لَكَ ذَلِكَ كُلَّهُ».
[صحيح] - [رواه مسلم] - [صحيح مسلم: 663]
المزيــد ...
Kutoka kwa Ubai bin Ka'ab radhi za Allah ziwe juu yake amesema:
Kulikuwa na mtu ambaye sifahamu kama kuna mtu alikuwa akiishi mbali kuliko yeye, na swala ilikuwa haimpiti, akaambiwa: Bora ungelinunua Punda ukimpanda nyakati za giza, na unapopita kwenye sehemu ya jangwa. Akasema: "Hainifurahishi nyumba yangu kuwa karibu na Msikiti, mimi ninapenda niandikiwe malipo ya kutembea kwangu, na kurudi kwangu ninaporejea kwa Watu wangu" Akasema Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani ziwe juu yake: "Hakika Mwenyezi Mungu amekukusanyia malipo yote hayo".
[Sahihi] - [Imepokelewa na Imamu Muslim] - [صحيح مسلم - 663]
Ameeleza Ubai bin Kaab radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake ya kwamba bwana mmoja katika Maanswari (watu wa Madina) alikuwa ni mtu anayeishi mbali kuliko wote kutoka ulipo Msikiti wa Mtume, na ilikuwa haimpiti swala yoyote; bali anahudhuria swala zote pamoja na Mtume rehema na amani ziwe juu yake, akaambiwa: Lau ungenunua punda wa kumpanda katika giza la usiku, na katika joto la Ardhi wakati wa mchana, akasema: Sipendezwi nyumba yangu kuwa karibu na msikiti, hakika mimi ninataka aniandikie Mwenyezi Mungu hatua zangu wakati wa kuja katika swala msikitini, na kurudi kwangu ninaporudi kwa watu wangu, yakafika maneno yake kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake akasema: "Hakika amekukusanyia Mwenyezi Mungu kwako yote hayo".