عن عبد الله بن عبَّاس رضي الله عنهما قال: «أُمِرَ الناس أن يكون آخر عَهْدِهِمْ بالبيت، إلا أنه خُفِّفَ عن المرأة الحائض».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abdillahi bin Abbas -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- Amesema "Waliamrishwa watu kuwe kuagana kwao kwa mwisho ni katika nyumba (Alka'ba), isipokuwa likaondoshwa hilo kwa mwanamke mwenye hedhi".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Nyumba tukufu inaheshima na takrima; yenyewe ni alama ya ibada za Mwenyezi Mungu na utulivu na unyenyekevu mbele yake yeye, ikapata heshima ndani ya vifua, na utukufu ndani ya nyoyo, na mapenzi na kufungamana nayo. Na kwaajili hiyo akamuamrisha Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- mwenye kuhiji iwe kuaga kwake ni hapo, na hii ndiyo twawafu (mzunguko) wa mwisho ambao ndio mzunguko wa kuaga, isipokuwa mwanamke mwenye hedhi; ni kwasababu huenda akauchafua msikiti kwa kuingia kwake, ikaondolewa kwake twawafu (mzunguko) bila kuufidia, na hii ni dalili katika hija hivyo haijumlishi na Umrah.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama