Aina:
+ -

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ:
«كُلُّ سُلَامَى مِنَ النَّاسِ عَلَيْهِ صَدَقَةٌ، كُلَّ يَوْمٍ تَطْلُعُ فِيهِ الشَّمْسُ تَعْدِلُ بَيْنَ الِاثْنَيْنِ صَدَقَةٌ، وَتُعِينُ الرَّجُلَ فِي دَابَّتِهِ فَتَحْمِلُهُ عَلَيْهَا أَوْ تَرْفَعُ لَهُ عَلَيْهَا مَتَاعَهُ صَدَقَةٌ، وَالكَلِمَةُ الطَّيِّبَةُ صَدَقَةٌ، وَكُلُّ خُطْوَةٍ تَمْشِيهَا إِلَى الصَّلَاةِ صَدَقَةٌ، وَتُمِيطُ الأَذَى عَنِ الطَّرِيقِ صَدَقَةٌ».

[صحيح] - [رواه البخاري ومسلم] - [الأربعون النووية: 26]
المزيــد ...

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Amesema Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-:
"Kila kiungo kwa mwanadamu kwake ni sadaka, kila siku linalochomoza jua ndani yake ukafanya uadilifu kati ya watu wawili hiyo ni sadaka, na ukamsaidia mtu katika kipando chake ukambeba au ukamnyanyulia mzigo ni sadaka, na neno zuri ni sadaka, na kila hatua unayopiga kwenda msikitini ni sadaka, na ukiondoa udhia barabarani nisadaka".

[Sahihi] - [رواه البخاري ومسلم] - [الأربعون النووية - 26]

Ufafanuzi

Mtume rehema na amani ziwe juu yake ameeleza kuwa kila Muislamu ni wajibu kila siku kuhesabu kila kiungo cha mifupa yake kuwa ni sadaka ya hiyari kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu na kuwa ni njia ya kumshukuru kwa neema ya afya, na kwamba amevifanya viungo vyake kuwa na maungio yanayomuwezesha kukunja na kukunjua, Sadaka hii inafanywa na matendo yote mema na haitegemei kutoa pesa, na miongoni mwake: Uadilifu wako na kusuluhisha kwako kati ya wagomvi wawili ni sadaka, Na katika kumsaidia kwako asiyejiweza kupanda katika mnyama wake, ukambeba, au ukamnyanyulia mzigo, ni sadaka. na neno zuri kuanzia kumtaja Mwenyezi Mungu na dua na salamu na mengineyo, ni sadaka, na kwa kila hatua unayoipiga kwenda katika swala, ni sadaka, na kuondoa kila yanayoudhi katika njia ni sadaka.

Katika Faida za Hadithi

  1. Muundo wa mifupa na viungo vya mwanadamu ni moja ya neema kubwa za Mwenyezi Mungu juu yake, hivyo kila mfupa peke yake unahitaji kutolewa sadaka kwa niaba yake ili itimie kushukuru neema hiyo.
  2. Himizo la kurudia upya shukurani kila siku ili neema hizo zidumu.
  3. Himizo la kudumu kufanya ibada za sunna na sadaka kila siku.
  4. Fadhila ya kusuluhisha baina ya watu.
  5. Himizo la mtu kumsaidia ndugu yake; kwani msaada wake kwake ni sadaka.
  6. Himizo la kuhudhuria swala za pamoja na kuziendea, na kuimarisha misikiti kwa hilo.
  7. Uwajibu wa kuheshimu njia wanazopita waumini kwa kuepuka yanayo waudhi au kuwadhuru.
Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Kibangali Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Thai German Pashto Kiassam Albanian الأمهرية الغوجاراتية Luqadda qer-qeesiya النيبالية الدرية الصربية الطاجيكية Luqadda kiniya ruwadiga المجرية التشيكية الموري الولوف Luqadda Asariga الأوزبكية الأوكرانية الجورجية المقدونية الخميرية
Kuonyesha Tarjama
Aina tofauti
Ziada