عن أبي موسى الأشعري رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : «إذا مَرِض العَبد أو سافر كُتِب له مثلُ ما كان يعمل مقيمًا صحيحًا».
[صحيح] - [رواه البخاري]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Musa Al Ash'ariy radhi za Mwenyezi ziwe juu yake Amesema: Amesema Mtume rehema na Amani zimfikie: "Atakapougua mja au akasafiri ataandikiwa malipo sawa na mfano wa yale aliyokuwa akiyafanya akiwa mkazi na mzima wa afya".
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy
Mtu itakapokuwa katika mazoea yake ni kufanya amali njema wakati wa afya yake na anapokuwa na nafasi, kisha akaugua akawa hakuweza kuifanya, basi yeye huandikiwa malipo kamili, kama jinsi ambavyo angefanya katika hali ya kuwa na afya, na hivyo hivyo itakapokuwa kilichomzuia ni safari au udhuru mwingine wowote kama hedhi.