عن أبي موسى الأشعري رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : «إذا مَرِض العَبد أو سافر كُتِب له مثلُ ما كان يعمل مقيمًا صحيحًا».
[صحيح] - [رواه البخاري]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Musa Al Ash'ariy radhi za Mwenyezi ziwe juu yake Amesema: Amesema Mtume rehema na Amani zimfikie: "Atakapougua mja au akasafiri ataandikiwa malipo sawa na mfano wa yale aliyokuwa akiyafanya akiwa mkazi na mzima wa afya".
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy

Ufafanuzi

Mtu itakapokuwa katika mazoea yake ni kufanya amali njema wakati wa afya yake na anapokuwa na nafasi, kisha akaugua akawa hakuweza kuifanya, basi yeye huandikiwa malipo kamili, kama jinsi ambavyo angefanya katika hali ya kuwa na afya, na hivyo hivyo itakapokuwa kilichomzuia ni safari au udhuru mwingine wowote kama hedhi.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Upana wa rehma za Mwenyezi Mungu Mtukufu na upole wake kwa waja wake.
  2. Atakayeshindwa kutekeleza yale aliyoyazoea katika matendo mema kwa udhuru wa kisheria au safari au maradhi pamoja na kusimama imara kwa nia ya kweli juu ya kufanya kwake wakati wa kuweza, ataandikiwa malipo yake kama jinsi ambavyo angekuwa mkazi na mzima wa afya.