عن سعيد بن المسيب عن أبيه المسيب بن حزن رضي الله عنه قال: "لما حضرَتْ أبا طالب الوفاة جاءه رسول الله صلى الله عليه وسلم وعنده عبد الله بن أبي أمية وأبو جهل، فقال له: يا عَمِّ قل لا إله إلا الله، كلمة أُحَاجُّ لك بها عند الله، فقالا له: أَتَرَغَبُ عن ملة عبد المطلب؟ فأعاد عليه النبي صلى الله عليه وسلم ، فأعادا، فكان آخر ما قال هو على ملة عبد المطلب، وأبى أن يقول لا إله إلا الله، فقال النبي صلى الله عليه وسلم : لأستغفرن لك ما لم أُنْهَ عنك، فأنزل الله: {مَا كَانَ لِلنَّبِيِّ وَالَّذِينَ آمَنُوا أَنْ يَسْتَغْفِرُوا لِلْمُشْرِكِينَ وَلَوْ كَانُوا أُولِي قربى...} الآية"، وأنزل الله في أبي طالب: {إِنَّكَ لا تَهْدِي مَنْ أَحْبَبْتَ وَلَكِنَّ اللَّهَ يَهْدِي مَنْ يَشَاءُ وَهُوَ أَعْلَمُ بِالْمُهْتَدِينَ}.
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Saidi bin Musayyib kutoka kwa baba yake Musayyib bin Hazmi -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: "Kilipomfikia Abuu Twalib kifo, Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- alimuendea naye kukiwa kwake kuna Abdullahi bin Abii Umaiyya na Abuu Jahli,Akasema kumwambia: Ewe baba mdogo, Sema Laa ilaaha illa llaah -Hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu-, neno ambalo nitakutetea kwalo kwa Mwenyezi Mungu, wakasema kumwambia: Unaichukia mila Abdul Muttwalib? Akamrudia tena Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- nao wakarudia, ikawa neno la mwisho alilotamka nikuwa yeye yuko katika mila ya Abdul Muttwalib, na akakataa kusema Laa ilaaha illa llaahu -Hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu-, akasema Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Hakika nitakuombea msamaha madamu sijakatazwa kukuombea, Akataremsha Mwenyezi Mungu: {Haikuwa kwa Nabii na wale walioamini kuwaombea msamaha washirikina hata kama watakuwa ndugu wa karibu...} Mpaka mwisho wa aya", Na akateremsha Mwenyezi Mungu kuhusu Abuu Twalib: {Hakika wewe humuongozi umtakaye, lakini Mwenyezi Mungu humuongoza amtakaye, naye ndiye mjuzi zaidi wa wale walioongoka}.
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Alimtembelea Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Abuu Twalib naye akiwa katika safari ya kifo na akamuwekea wazi kuhusu uislamu; ili uwe ndio mwisho wa maisha yake ili apate kupitia hilo mafanikio na utukufu, na akamtaka aseme neno la tauhidi (la kumpwekesha Mwenyezi Mungu), na wakamtaka washirikina abakie katika dini ya baba zake ambayo ni ushirikina; kwa maarifa yao juu ya kile kinachomaanishwa na neno hili ikiwemo kupinga ushirikina na kutakasa ibada kwaajili ya Mwenyezi Mungu pekee, na akurudia Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kuomba kutamka shahada kutoka kwa Ammi yake (baba yake mdogo), na wakarudia washirikina upinzani na ikawa ndiyo sababu ya kumzuia katika haki na kufa kwake katika ushirikina. Na hapo ndipo alipoapa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kuwa atamtafutia kwa Mwenyezi Mungu msamaha madamu hajazuiwa kwa hilo, akateremsha Mwenyezi Mungu zuio la kumuombea na akambainishia kuwa uongofu uko mkononi mwa Mwenyezi Mungu anamtunuku amtakaye; kwasababu yeye anajua ni nani anayestahiki na asiyestahiki. Akateremsha Mwenyezi Mungu Aliyetakasika na Kutukuka: "Hakika wewe humuongozi umtakaye lakini Mwenyezi Mungu anamuongoza amtakaye naye ndiye mjuzi zaidi wa wale walioongoka".

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Pashto Kiassam السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama
Ziada