عن عبد الله بن عباس رضي الله عنهما قال: "ما السماوات السبع والأرضون السبع في كَفِّ الرحمن إلا كَخَرْدَلَةٍ في يد أحدكم".
[نقل الألباني تصحيحه عن ابن تيمية ولم يتعقبه] - [رواه عبد الله بن الإمام أحمد لكن بلفظ: "في يد الله" وابن جرير الطبري والذهبي]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abdillah bin Abbasi -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- Amesema: "Si chochote mbingu saba na ardhi saba katika kiganja cha Ar-Rahmaani -Mwingi wa rehema- isipokuwa ni kama punje ya ulezi katika mkono wa mmoja wenu".
Albany amenukuu usahihi wake kutoka kwa Ibn Taymiyyah na hakuifatilia - Imepokelewa na Ibnu Jariri

Ufafanuzi

Anatueleza Abdillahi bin Abbasi -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- katika nukuu hii kuwa kiwango cha asilimia ya mbingu saba na ardhi saba pamoja na ukubwa wake katika kiganja cha Ar-Rahmaani -Mwingi wa Rehema-, ni kama kiwango cha punje ndogo ya ulezi katika kiganja cha mmoja wetu, na hii ni kufananisha kiwango kwa kiwango, na si kufananisha kiganja kwa kiganja; kwasababu Mwenyezi Mungu sifa zake hazifanani na kitu chochote kama ambavyo dhati yake haifanani na chochote.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama