عن عبد الله بن عمر رضي الله عنهما قال: «صَلَّيتُ معَ رسول الله -صلَّى الله عليه وسلم- رَكعَتَين قَبل الظُّهر، وَرَكعَتَين بَعدَها، ورَكعَتَين بعد الجُمُعَةِ، ورَكعَتَينِ بَعدَ المَغرِب، وَرَكعَتَينِ بَعدَ العِشَاء». وفي لفظ: «فأمَّا المغربُ والعشاءُ والجُمُعَةُ: ففي بَيتِه». وفي لفظ: أنَّ ابنَ عُمَر قال: حدَّثَتنِي حَفصَة: أنَّ النبِيَّ -صلَّى الله عليه وسلم-: «كان يُصَلِّي سَجدَتَين خَفِيفَتَينِ بَعدَمَا يَطلُعُ الفَجر، وكانت سَاعَة لاَ أَدخُلُ على النبيَّ -صلَّى الله عليه وسلم- فِيهَا».
[صحيح] - [متفق عليه بجميع رواياته]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abdillahi bin Omar -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- Amesema: "Nilisali pamoja na Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- rakaa mbili kabla ya adhuhuri, na rakaa mbili baada yake, na rakaa mbili baada ya Ijumaa, na rakaa mbili baada ya magharibi, na rakaa mbili baada ya ishaa" Na katika lafudhi nyingine: "Na ama magharibi na ishaa na ijumaa: hizo aliswalia nyumbani". Na katika tamko lingine: Nikuwa Bin Omar alisema: Alinisimulia Hafswa: kuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake-: "Alikuwa akisali sijida mbili nyepesi (fupi) baada ya kuchomoza alfajiri, na zilikuwa ni nyakati ambazo siingii kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake-".
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy na Muslim katika riwaya zake zote

Ufafanuzi

Katika hadithi hii kuna ubainifu wa sunna zilizo na mpangilio za swala tano, nayo nikuwa; adhuhuri ina rakaa nne, rakaa mbili kabla yake, na rakaa mbili baada yake, nakuwa swala ya ijumaa ina rakaa mbili baada yake, nakuwa magharibi ina rakaa mbili baada yake, nakuwa swala ya ishaa ina rakaa mbili baada yake, nakuwa sunna zenye mpangilio kwa swala za usiku, magharibi na ishaa, na sunna za alfajiri na ijumaa alikuwa akiziswali Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- nyumbani kwake. Na alikuwa bin Omar -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- na mawasiliano na nyumba ya Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake-; kwasababu ya nafasi ya dada yake "Hafswa" kwa Nabii -Rehema na Amani ziwe juu yake- akawa anaingia kwake katika nyakati zake za ibada, lakini alikuwa na adabu haingii baadhi ya nyakati, ambazo hakuna ruhusa ya kuingia kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kwa kutekeleza kauli yake Mtukufu: "Enyi mlioamini wakutekeni idhini wale iliomiliki mikono yenu ya kulia, wale ambao bado hawajafikia balehe, mara tatu, kabla ya swala ya alfajiri" mpaka mwisho wa aya, akawa haingii kwake katika nyakati ambazo ziko kabla ya alfajiri, ili aone ni namna gani alikuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- akiswali, lakini, kutokana na pupa yake juu ya elimu alikuwa akimuuliza dada yake (Hafswa) kuhusu hilo, anamueleza kuwa Nabii -Rehema na Amani ziwe juu yake- Alikuwa akiswali sijida mbili nyepesi baada ya kuchomoza alfajiri, nazo ni sunna ya swala ya alfajiri.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Thai Pashto Kiassam السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama