عن أبي هريرة رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : (لولاَ أن أَشُقَّ عَلَى أُمَّتِي؛ لَأَمَرتُهُم بِالسِّوَاك عِندَ كُلِّ صَلاَة).
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Amesema Mjumbe wa Mwenyezi Mungu -Rehema na Amani ziwe juu yake-: "Laiti nisingeliogopea uzito kwa umma wangu; ningeliwaamrisha kupiga mswaki kila wakati wa swala"
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Katika ukamilifu wa nasaha za Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- na kuupendelea kwake kheri umma wake, na hamu yake ya kutaka wafanye kila kitendo ambacho maslahi yake yanarudi kwao; ili wapate utukufu kamili nikuwahamasisha kwake juu ya kupiga mswaki, na kuwa yeye -Rehema na Amani ziwe juu yake- alipojua wingi wa faida za mswaki, na athari ya manufaa yake sasa hivi na baadaye; alikaribia kuulazimisha umma wake juu ya hilo kila wakati wa udhu au wa swala; kwa kupokelewa riwaya ya: (pamoja na kila udhu), lakini kwa ukamilifu wa huruma yake na upole wake alihofia huenda Mwenyezi Mungu akauwajibisha juu yao; wakashindwa kuutekeleza; wakapata dhambi; akaacha ili usifaradhishwe kwao kwa kuwahofia na kuwahurumia, lakini pamoja na hili amewahamasisha na akawahimiza juu yake.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama