عن أبي هريرة رضي الله عنه قال: كان رسول الله صلى الله عليه وسلم إذا عطس وضع يده أو ثوبه على فيه، وخفض -أو غض- بها صوته، شك الراوي.
[صحيح] - [رواه أبو داود والترمذي وأحمد]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Alikuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- anapopiga chafya anaweka mkono wake au nguo yake juu ya kinywa chake, na anapunguza -au anazuia- sauti yake, hapa kuna shaka kwa mpokezi.
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Tirmidhiy

Ufafanuzi

Imeonyesha hadithi juu ya adabu miongoni mwa adabu zinazohusiana na chafya, ni sunna kwa mwenye kupiga chafya asipitilize katika kupiga chafya na asinyanyue sauti yake, bali aipunguze na afunike uso wake ikiwezekana.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kichina Kifursi Kihindi Kisin-hala Kikurdi Kihausa Kireno الدرية
Kuonyesha Tarjama