عن حذيفة بن اليمان رضي الله عنهما قال: «كان رسول الله صلى الله عليه وسلم إِذَا قَام من اللَّيل يُشُوصُ فَاهُ بِالسِّوَاك».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Hudhaifa bin Yamani -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- Amesema: "Alikuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- anapoamka asubuhi anasukutua kinywa chake kwa mswaki"
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Katika mapenzi ya Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake ya usafi na kuchukia kwake harufu mbaya nikuwa yeye alikuwa anapoamka kutoka katika usingizi mrefu ambao ndio unadhaniwa kuwa sababu ya kubadilika kwa harufu ya mdomo, alikuwa akisugua meno yake -Rehema na Amani ziwe juu yake- kwa mswaki, ili akate harufu mbaya, na ili achangamke baada ya usingizi kuzidi kusimama kwake; kwasababu katika mambo maalumu kwa mswaki pia ni kuzindua na kuchangamsha.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama