عن أبي هريرة رضي الله عنه مرفوعاً: «الفِطرة خَمْسٌ: الخِتَان، والاسْتِحدَاد، وقَصُّ الشَّارِب، وتَقلِيمُ الأَظفَارِ، ونَتْفُ الإِبِط».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira radhi za Mwenyezi Mungu zimfikie, hadithi marfu'u: "Mambo ya kimaumbile ni matano: Kutairiwa, na kuondoa nywele za sehemu ya siri, na kupunguza masharubu, na kupunguza kucha, na kukwapua nywele za kwapani"
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Anaeleza Abuu Huraira radhi za Mwenyezi Mungu zimfikie yakwaba yeye alimsikia Mtume rehema na Amani ziwe juu yake Akisema: Mambo matano ni katika dini ya uislamu, Ambayo aliwaumba nayo Mwenyezi Mungu, Atakayeyatekeleza, basi atakuwa kafanya mambo makubwa katika dini takatifu. Na haya matano yaliyotajwa katika hadithi, ni sehemu ya usafi, ambao uislamu ulikuja nao. La kwanza: Ni kukata ngozi ya uume, ambayo kubaki kwake kunasababisha mrundikano wa najisi na uchafu unaoweza kuzusha maradhi na vidonda. La pili: Ni kunyoa nywele zilizo pembezoni mwa utupu, sawasawa uwe ni utupu wa mbele au nyuma, kwasababu kubakia mahala pake kunasababisha kujichafua kwa najisi, na huenda zikaharibu twahara (usafi) wa kisheria. La Tatu: Kupunguza masharubu, ambayo kubaki kwake kunasababisha kuharibika muonekano wa umbile, na ni karaha kunywa katika chombo alichokitumia mwenye masharubu, nayo ni katika kujifananisha na majusi (wanao abudu moto). La nne: Kupunguza makucha, ambayo kubaki kwake kunasababisha kukusanyika kwa uchafu ndani yake, yakajitokeza maradhi. Na pia huenda yakazuia ukamilifu wa twahara kwa kuziba kwake baadhi ya sehemu za faradhi. La Tano: Kukwapua nywele za kwapani, ambazo kubaki kwake kunasababisha harufu mbaya.

Kufanya Tarjama: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibaghali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese German Kijapani
Kuonyesha Tarjama

Faida nyingi

  1. Asili ya Umbile aliloumba Mwenyezi Mungu linapelekea katika kila kheri na linaepusha na kila shari.
  2. Mambo ya kimaumbile ni matano, idadi hii si ya kudhibiti kwamba ni hayo tu, kwasababu maana ya idadi si hoja, na imekuja katika sahihi Muslim kuwa: Mambo kumi ni katika maumbile.
  3. Ni sheria kuyazingatia mambo haya, na kutojisahau nayo.
  4. Mambo haya matano matukufu, ni katika maumbile aliyoumba Mwenyezi Mungu, ambayo anayapenda na anayaamrisha. Na akawasisitiza watu wenye kujitambua juu ya mambo hayo na akawaepushia yasiyokuwa hayo.
  5. Dini ya Uislamu ilikuja na usafi na uzuri na ukamilifu.
  6. Na katika mambo haya kuna faida za kidini na kidunia, miongoni mwazo ni: Kupendezesha muonekano na kusafisha mwili, na udharura wa usafi, na kwenda kinyume na alama za makafiri na kutekeleza amri ya sheria.
  7. Wanayoyafanya siku hizi baadhi ya vijana wa kiume na wa kike katika kufuga makucha, na wanayoyafanya baadhi ya wanaume katika kuachia masharubu, yote haya ni katika mambo yaliyokatazwa kisheria, yasiyopendeza hata kiakili na kihisia, uislamu hauamrishi ispokuwa kila zuri na wala haukatazi ispokuwa kila baya, ispokuwa kuwaiga wazungu kiupofu ndiko kumegeuza uhalisia na kukapendezesha mambo mabaya, na kukapoteza uzuri kiakili na kihisia na kisheria.