عن أبي هريرة رضي الله عنه مرفوعاً: «الفِطرة خَمْسٌ: الخِتَان، والاسْتِحدَاد، وقَصُّ الشَّارِب، وتَقلِيمُ الأَظفَارِ، ونَتْفُ الإِبِط».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Huraira radhi za Mwenyezi Mungu zimfikie, hadithi marfu'u: "Mambo ya kimaumbile ni matano: Kutairiwa, na kuondoa nywele za sehemu ya siri, na kupunguza masharubu, na kupunguza kucha, na kukwapua nywele za kwapani"
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim
Anaeleza Abuu Huraira radhi za Mwenyezi Mungu zimfikie yakwaba yeye alimsikia Mtume rehema na Amani ziwe juu yake Akisema: Mambo matano ni katika dini ya uislamu, Ambayo aliwaumba nayo Mwenyezi Mungu, Atakayeyatekeleza, basi atakuwa kafanya mambo makubwa katika dini takatifu. Na haya matano yaliyotajwa katika hadithi, ni sehemu ya usafi, ambao uislamu ulikuja nao. La kwanza: Ni kukata ngozi ya uume, ambayo kubaki kwake kunasababisha mrundikano wa najisi na uchafu unaoweza kuzusha maradhi na vidonda. La pili: Ni kunyoa nywele zilizo pembezoni mwa utupu, sawasawa uwe ni utupu wa mbele au nyuma, kwasababu kubakia mahala pake kunasababisha kujichafua kwa najisi, na huenda zikaharibu twahara (usafi) wa kisheria. La Tatu: Kupunguza masharubu, ambayo kubaki kwake kunasababisha kuharibika muonekano wa umbile, na ni karaha kunywa katika chombo alichokitumia mwenye masharubu, nayo ni katika kujifananisha na majusi (wanao abudu moto). La nne: Kupunguza makucha, ambayo kubaki kwake kunasababisha kukusanyika kwa uchafu ndani yake, yakajitokeza maradhi. Na pia huenda yakazuia ukamilifu wa twahara kwa kuziba kwake baadhi ya sehemu za faradhi. La Tano: Kukwapua nywele za kwapani, ambazo kubaki kwake kunasababisha harufu mbaya.