+ -

عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ رَضيَ اللهُ عنهُ قَالَ:
وُقِّتَ لَنَا فِي قَصِّ الشَّارِبِ، وَتَقْلِيمِ الْأَظْفَارِ، وَنَتْفِ الْإِبِطِ، وَحَلْقِ الْعَانَةِ، أَلَّا نَتْرُكَ أَكْثَرَ مِنْ أَرْبَعِينَ لَيْلَةً.

[صحيح] - [رواه مسلم] - [صحيح مسلم: 258]
المزيــد ...

Imepokelewa kutoka kwa Anas bin Maalik -radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- amesema:
Tuliwekewa muda wa kupunguza sharubu, na kupunguza kucha, na kung'oa nywele za kwapa, na kunyoa nywele za siri, tusiziache zaidi ya siku arobaini.

[Sahihi] - [Imepokelewa na Imamu Muslim] - [صحيح مسلم - 258]

Ufafanuzi

Aliweka kikomo Mtume rehema na amani ziwe juu yake cha mtu kupunguza sharubu, na kupunguza kucha za mikono na miguu, na kung'oa nywele za kwapa, na kunyoa nywele za siri, kusizidi kuziacha kwake zaidi ya siku arobaini.

Katika Faida za Hadithi

  1. Amesema Shaukani: Kilicho sawa nikuwa adhibiti kwa arobaini aliyoidhibiti kwayo Mtume rehema na amani ziwe juu yake haitakiwi kuivuka, na haitochukuliwa kama kwenda kinyume na sunna kwa kuacha kupunguza na mfano wake baada kurefuka mpaka ifike kikomo cha muda huo.
  2. Amesema bin Hubaira: Hadithi hii ndio kikomo cha kuchelewesha hilo, na kilichobora ni kulitekeleza hilo kabla ya ukomo huo.
  3. Uislamu umetilia kipaumbele usafi na kujitwaharisha na kujipamba.
  4. Kupunguza sharubu, kwa kunyoa nywele zinazoota juu ya mdomo wa juu.
  5. Kukwapua nywele za kwapa, kwa kuondoa nywele zinazoota humo, nayo ni sehemu inayokuwa chini ya maungio kati ya mkono na bega.
  6. Kunyoa nywele za siri, nazo ni nywele zinazoota pembezoni mwa tupu ya mbele, kwa mwanaume na mwanamke.
Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiindonesia Kisin-hala Kivetenamu Kihausa Kiassam الهولندية الغوجاراتية الرومانية المجرية الجورجية
Kuonyesha Tarjama