عن عائشة رضي الله عنها : أن النبي صلى الله عليه وسلم قال: «السِّواك مَطْهَرَةٌ للْفَم مَرْضَاةٌ لِلرَّبِّ».
[صحيح] - [رواه النسائي وأحمد والدارمي]
المزيــد ...

Kutoka kwa Aisha -Radhi za Allah ziwe juu yake- Yakwamba Mtume- Rehma na amani ziwe juu yake- amesema: "Mswaki ni kisafisha kinywa na humridhisha Mola".
Sahihi - Imepokelewa na An-Nasaaiy

Ufafanuzi

Mswaki husafisha kinywa kutokana na uchafu na harufu mbaya na mengineyo yanayo dhuru, na kwa chochote atakachopigia mtu katika vile vinavyoondoa mabadiliko atakuwa kapatia sunna ya mswaki, kama ambavyo akisafisha meno yake kwa brashi na dawa ya meno, na vinginevyo katika vile vinavyoondoa uchafu, nao unamridhisha Mola, Yaani nikuwa kupiga mswaki ni katika sababu za kumridhisha Mwenyezi Mungu Mtukufu kutoka kwa mja. Na wametaja faida nyingine nyingi kuhusu mswaki, miongoni mwazo ni: Hupendezesha kinywa, na huzipa nguvu fizi, na hung'arisha macho, na huondoa makohozi, na huenda sambamba na mafundisho, na huwafurahisha Malaika, na huzidisha uzuri, na hurekebisha utumbo.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Nikuwa mswaki ni njia ya kusafisha kinywa.
  2. Mwenyezi Mungu Mtukufu anapenda usafi na anawapenda wenye kujisafisha, ndio maana akawawekea sheria kwa yale yatakayo wasaidia kutafuta radhi zake.
  3. Ubora wa mswaki.
  4. Kuuhimiza Mtume rehema na Amani zimfikie umma wake kukithirisha kupiga mswaki.
  5. Ni sheria kupiga mswaki kwa aliyefunga sawa sawa iwe mwanzo mchana au mwisho wake; kwa uwazi wa hadithi.
  6. Kupiga mswaki ni katika sababu za kumridhisha Mwenyezi Mungu Mtukufu kutoka kwa mja.
  7. Kuthibitisha sifa ya kuridhia kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu.