عن عائشة رضي الله عنها : أن النبي صلى الله عليه وسلم قال: «السِّواك مَطْهَرَةٌ للْفَم مَرْضَاةٌ لِلرَّبِّ».
[صحيح] - [رواه النسائي وأحمد والدارمي]
المزيــد ...
Kutoka kwa Aisha -Radhi za Allah ziwe juu yake- Yakwamba Mtume- Rehma na amani ziwe juu yake- amesema: "Mswaki ni kisafisha kinywa na humridhisha Mola".
Sahihi - Imepokelewa na An-Nasaaiy
Mswaki husafisha kinywa kutokana na uchafu na harufu mbaya na mengineyo yanayo dhuru, na kwa chochote atakachopigia mtu katika vile vinavyoondoa mabadiliko atakuwa kapatia sunna ya mswaki, kama ambavyo akisafisha meno yake kwa brashi na dawa ya meno, na vinginevyo katika vile vinavyoondoa uchafu, nao unamridhisha Mola, Yaani nikuwa kupiga mswaki ni katika sababu za kumridhisha Mwenyezi Mungu Mtukufu kutoka kwa mja. Na wametaja faida nyingine nyingi kuhusu mswaki, miongoni mwazo ni: Hupendezesha kinywa, na huzipa nguvu fizi, na hung'arisha macho, na huondoa makohozi, na huenda sambamba na mafundisho, na huwafurahisha Malaika, na huzidisha uzuri, na hurekebisha utumbo.