عن عائشة رضي الله عنها قالت: «كان رسول الله صلى الله عليه وسلم يعجبه التيمُّن في تَنَعُّلِّه، وترجُّلِه، وطُهُورِه، وفي شَأنه كُلِّه».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Aisha -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: "Alikuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kukimpendeza sana kuanzia kulia katika kuvaa kwake viatu, na kuchana kwake nywele, na twahara yake, na katika mambo yake yote."
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Anatueleza Aisha -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kuhusu mazoea ya Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- yanayopendeka kwake, nayo ni kutanguliza kulia katika kuvaa viatu vyake, na kuchana nywele zake, na kuziachanisha kwake, na kujisafisha kwake kutokana na uchafu, na katika mambo yake yote ambayo ni katika hayo yaliyotajwa kama kuvaa kanzu na suruali, na kulala, na kula na kunywa na mfano wa hayo. Yote haya ni katika sehemu ya kujipa matumaini mazuri na kuutukuza upande wa kulia kuliko wa kushoto; na kwasababu hii alikataza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kustanji kwa mkono wa kulia, na akakataza kushika uume kwa mkono wa kulia, kwasababu kulia ni kwaajili ya vitu vizuri, na kushoto kwa yasiyokuwa hayo.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo
Kuonyesha Tarjama