+ -

عَنْ وَائِل بن حُجرٍ رضي الله عنه قَالَ:
صَلَّيْتُ مَعَ النَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ، فَكَانَ يُسَلِّمُ عَنْ يَمِينِهِ: «السَّلَامُ عَلَيْكُمْ وَرَحْمَةُ اللَّهِ وَبَرَكَاتُهُ»، وَعَنْ شِمَالِهِ: «السَّلَامُ عَلَيْكُمْ وَرَحْمَةُ اللَّهِ».

[حسن] - [رواه أبو داود] - [سنن أبي داود: 997]
المزيــد ...

Kutoka kwa Waili bin Hujari radhi za Allah ziwe juu yake amesema:
Niliswali pamoja na Mtume rehema na amani ziwe juu yake, alikuwa akitoa salaam kuliani kwake: "Assalaam alaikum warahamatullah wabarakaatuh", na kushotoni kwake: "Assalaam alaikum warahmatullah".

[Ni nzuri] - [Imepokelewa na Abuu Daud] - [سنن أبي داود - 997]

Ufafanuzi

Alikuwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake anapotaka kumaliza swala yake anatoa salaam kuliani kwake na kushotoni kwake kwa kugeuka kwa uso wake upande wa kulia, pamoja na kusema: "Assalaam alaikum warahmatullaahi wabarakaatuh", na anatoa salaam kushotoni kwake, kwa kugeuza uso wake upande wa kushoto, pamoja na kusema: "Assalaam alaiku warahmatullah".

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kireno Kiassam الهولندية الغوجاراتية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Sheria ya kutoa salaam mbili ndani ya swala, nakuwa salam hizo ni katika nguzo zake.
  2. Inapendeza kuleta ziada ya kauli "wabarakaatuh", katika baadhi ya nyakati; kwa sababu Mtume rehema na amani ziwe juu yake hakuwa anadumu nayo.
  3. Kutamka salaam mbili ndani ya swala ni nguzo ya wajibu, na ama kitendo cha kugeuka wakati wa kuzitamka ni sunna.
  4. Inatakiwa iwe kauli ya: "Assalaam alaikum warahmatullaah" wakati wa kitendo cha kugeuka na si kabla yake wala baada yake.