عن ابن عباس رضي الله عنهما عن النبي صلى الله عليه وسلم قال: «أمِرْت أن أسْجُد على سَبْعَة أعَظُم على الجَبْهَة، وأشار بِيَده على أنْفِه واليَدَين والرُّكبَتَين، وأطْرَاف القَدَمين ولا نَكْفِتَ الثِّياب والشَّعر».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...
Kutoka kwa bin Abbas -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- Kutoka kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Nimeamrishwa nisujudu kwa viungo saba,paji la uso, na akaashiria kwa mkono wake katika pua yake, na mikono miwili na magoti mawili, na ncha za miguu miwili,na wala tusizikunje nguo na nywele".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim
Maana ya hadithi: "Nimeamrishwa nisujudu" Na katika riwaya nyingine "Tumeamrishwa": Na katika riwaya nyingine "Ameamrisha Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake-; Na riwaya zote tatu ni za Imamu Bukhariy, na kanuni ya kisheria nikuwa: Alichoamrishwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- hicho ni amri kwake na kwa umma wake; "makusudio ya viungo saba": Yaani: nimeamrishwa nisujudu juu ya viungo saba, katika hadithi imetajwa mifupa; makusudio ya mifupa ni viungo vya kusujudia, kama ilivyokuja imetafsiriwa katika riwaya nyingine, kisha akavifafanua kwa kauli yake "Juu ya paji la uso" Yaani nimeamrishwa nisujudu kwa paji la uso, pamoja na pua kama inavyoonyesha kauli yake: "Na akaashiria katika pua yake", Yaani akaashiria katika pua yake ili aweke wazi kuwa hicho ni kiungo kimoja. "Na mikono miwili" Yaani na ndani ya viganja vyake, kama jinsi inavyokusudiwa hivyo kwa ujumla , "Na magoti mawili na ncha za miguu miwili" Yaani: Na nimeamrishwa nisujudu kwa magoti mawili na juu ya ncha za vidole vya miguu miwili, na katika hadithi ya Abii Humaidi As sa'idiy- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- katika kuelezea sifa ya swala kwa tamko: (Na akaelekea kwa vidole vya miguu yake kibla) Yaani: naye akiwa kasujudu. "Na tusikunje nguo na nywele" Maana yake: tusikusanye wala tusikunje nguo na nywele kwasababu ya kusambaa wakati wa kurukuu na kusujudu, bali tuliache jambo katika hali yake kama lilivyo, ili mtu aporomoke katika ardhi na asujudu kwa viungo vyote na nguo na nywele.