عن عبد الله بن عمر رضي الله عنهما أن النبي صلى الله عليه وسلم كان يرفع يديه حَذْوَ مَنْكِبَيْهِ إذا افْتَتَحَ الصلاة، وإذا كبّر للرُّكُوعِ ، وإذا رفع رأسه من الركوع رَفَعَهُمَا كذلك، وقال: سَمِعَ الله لمن حَمِدَهُ رَبَّنَا ولك الحمد، وكان لا يفعل ذلك في السُّجُودِ.
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abdillahi bin Omar -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- Yakwamba Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Alikuwa akinyanyua mikono yake usawa wa mabega yake anapofungua swala, na anapotoa takbira ya kurukuu, na anaponyanyua kichwa chake kutoka katika rukuu anainyanyua pia, na akasema: "Sami'a llaahu liman hamidahu" Yaani: Amemsikia Mwenyezi Mungu yule aliyemuhimidi, "Rabbanaa walakal hamdu" Mola wetu na sifa njema ni zako, na alikuwa hafanyi hivyo katika sijida.
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Swala ni ibada tukufu, hivyo kila kiungo katika mwili ndani ya swala kina ibada yake maalumu. Na miongoni mwa hivyo ni mikono miwili ina kazi yake, miongoni mwake ni kuinyanyua wakati wa takbira ya kuhirimia swala (ya kuanza swala) na kuinyanyua ni pambo la swala na ni kumtukuza Mwenyezi Mungu -Mtukufu-, na kunakuwa kunyanyua mikono miwili kunalingana na mabega mawili, na kuinyanyua pia kwaajili ya rukuu katika rakaa zote, na anaponyanyua kichwa chake kutoka katika rukuu katika kila rakaa, na katika hadithi hii kaweka wazi mpokezi kuwa; Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- hafanyi hivyo katika sijida kiasi ambacho yeye aliporomoka na akashuka.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno الدرية
Kuonyesha Tarjama