عن أَنَس بن مالك رضي الله عنه عَنْ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: «اعْتَدِلُوا في السجود، ولا يَبْسُطْ أحدكم ذِرَاعَيْهِ انْبِسَاطَ الكلب».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Anas bin Maliki -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Linganeni sawa katika sijida, na asikunjue mmoja wenu mikono yake kama anavyokunjua mbwa".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Ameamrisha Nabii -Rehema na Amani ziwe juu yake- kulingana katika sijida, na hii nikuwa, ili mwenye kuswali awe na muonekano mzuri katika sijida, kiasi kwamba aweke viganja vyake katika ardhi, na anyanyue miundi yake na aiweke mbali na mbavu zake, kwasababu hali hii ndio anuani ya uchangamfu na hamu vinavyohitajika ndani ya swala, na ni kwasababu muonekano huu mzuri unaviwezesha viungo vya kusujudu vyote kuchukua nafasi yake katika ibada. Na akakatazwa kunyoosha mikono miwili katika sijida; kwasababu hii ni dalili ya uvivu na uchovu, na kuna kujifananisha na mbwa, nako nikujifananisha na kisichofaa.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama