عن أبي هريرة رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم قال: ألا أُحَدِّثُكُمْ حديثا عن الدجال ما حدَّثَ به نبيٌّ قومه! إنه أعور، وإنه يَجيءُ معه بمثالِ الجنة والنار.
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: Hivi nikuhadithieni hadithi kuhusu Dajali ambayo hajawahi kuhadithia Nabii yeyote watu wake! Hakika yeye ni chongo, na hakika yeye atakuja akiwa pamoja na mfano wa pepo na moto, anayoisema kuwa ni pepo huo ndio moto.
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Hakuna Nabii yeyote katika Manabi isipokuwa aliwatahadharisha watu wake na Dajali mwenye chongo, nakuwa yeye hatokuja isipokuwa zama za mwisho, Ama Mtume wetu -Rehema na Amani ziwe juu yake- yeye kaweka wazi kuhusu dajali kwa yale ambayo hawakuwahi kuyasema Mitume na Manabii kabla yake, nakuwa yeye atawazuga watu, na atawachanganya watadhania kuwa huyu aliyemtii kamuingiza peponi, nakuwa huyu aliyemuasi kamuingiza motoni, na uhalisia ni kinyume na hivyo.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno الدرية
Kuonyesha Tarjama