عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بن مسعودٍ رضي الله عنه قَالَ: سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَقُولُ:
«إِنَّ مِنْ شِرَارِ النَّاسِ مَنْ تُدْرِكُهُ السَّاعَةُ وَهُمْ أَحْيَاءٌ، وَمَنْ يَتَّخِذُ الْقُبُورَ مَسَاجِدَ».

[حسن] - [رواه أحمد] - [مسند أحمد: 3844]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abdallah bin Masoud -Radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Nilimsikia Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- akisema:
"Hakika katika watu waovu zaidi ni wale watakaokutwa na Kiyama wakiwa hai, na mwenye kuyafanya makaburi kuwa mahala pa kusalia".

[Ni nzuri (Hasan)] - [Imepokelewa na Ahmad] - [Musnad wa Ahmad - 3844]

Ufafanuzi

Anaeleza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuhusu watu waovu, nakuwa hao ndio Kiyama kitasimama juu yao, na wale wanaoyafanya makaburi kuwa misikiti, wakisali hapo na wakiyaelekea wakati wa ibada.

Katika Faida za Hadithi

  1. Uharamu wa kujenga misikiti juu ya makaburi; kwa sababu kitendo hicho ni njia ya kuingia katika shirki.
  2. Uharamu wa kusali katika makaburi hata bila kujengea; kwa sababu msikiti ni jina la kila mahali panaposujudiwa hapo hata kama hakuna jengo.
  3. Atakayeyafanya makaburi ya watu wema kuwa mahala pa kusalia huyo ni katika viumbe waovu, hata kama atadai kuwa lengo lake ni kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu.
Kuonyesha Tarjama
Lugha: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Ziada (56)