عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بن مسعودٍ رضي الله عنه قَالَ: سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَقُولُ:
«إِنَّ مِنْ شِرَارِ النَّاسِ مَنْ تُدْرِكُهُ السَّاعَةُ وَهُمْ أَحْيَاءٌ، وَمَنْ يَتَّخِذُ الْقُبُورَ مَسَاجِدَ».  
                        
[حسن] - [رواه أحمد] - [مسند أحمد: 3844]
                        
 المزيــد ... 
                    
Kutoka kwa Abdallah bin Masoud -Radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Nilimsikia Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- akisema:
"Hakika katika watu waovu zaidi ni wale watakaokutwa na Kiyama wakiwa hai, na mwenye kuyafanya makaburi kuwa mahala pa kusalia". 
                                                     
                                                                                                    
[Ni nzuri] - [Imepokelewa na Ahmad] - [مسند أحمد - 3844]                                            
Anaeleza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuhusu watu waovu, nakuwa hao ndio Kiyama kitasimama juu yao, na wale wanaoyafanya makaburi kuwa misikiti, wakisali hapo na wakiyaelekea wakati wa ibada.